11 Aprili 2019

Jeshi la sudan lakalia kiti kuiondoza sudan

Omar al bashir nje ya kiti.
Sudan kimenuka baada ya waandamanaji wakimshinikiza ya Omar Bashir ambaye ameiongoza sudani kwa miaka 31

10 Aprili 2019

Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ajiandaa kuiongoza tena Israel kwa muhula ujao

Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akatetea nafasi yake katika muhula wa tano
Chama chake Likud na washirika wake wa mrengo wa kulia wanatarajiwa kujizolea viti 65 kati ya 120 vya bunge, vyombo vya habari nchini humo vimeeleza.
Waziri Mkuu huyo mwenye miaka 69 anakabiliwa na shutuma za rushwa
Hata hivyo, matokeo ya uchaguzi yana maana kuwa atakuwa waziri kuu aliyekaa madarakani kwa muda mrefu, akimzidi baba wa taifa hilo David Ben-Gurion.
Netanyahu amesema ''Nimeguswa sana kwa namna watu walivyoniamini kwa mara ya tano, na kuahidi kunipa kura nyingi kuliko kura zilizopita''
''Nina nia ya kuwa waziri mkuu wa wananchi wote wa Israel.Wa mrengo wa kulia, kushoto, wayahudi, wasio wayahudi.Raia wote.''Alisema Netanyahu.
Kampeni zilivyofanyika
Netanyahu ametoa ujumbe mzito kuhusu masuala ya usalama kabla ya kupiga kura, suala lililogeuka kuwa moja kati ya masuala muhimu katika uchaguzi huo.
Alitoa tangazo muhimu katika siku za mwisho za kampeni, akieleza kuwa serikali mpya itaondoa makazi ya wayahudi kwenye ukingo wa magharibi
Makazi hayo yanatajwa kuwepo kinyume cha sheria, chini ya sheria za kimataifa, ingawa Israel imekua ikipinga hilo.
Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na Luteni Jenerali mstaafu Benny GantzHaki miliki ya pichaAFP
Image caption
Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na Luteni Jenerali mstaafu Benny Gantz
Katika hatua nyingine upinzani umekishutumu chama cha Likud kwa kupeleka waangalizi 1,200 wanaodaiwa kuwa na Kamera za siri ndani ya vituo vya kupigia kura,katika maeneo ya jamii za kiarabu.
Muungano wa jamii ya kiarabu,Hadash-Taal,umesema kuwa kitendo hicho ni kinyume cha ''sheria'' ambacho kina nia ya kuwatisha waarabu, lakini chama cha Likud kimesema kilitaka kuwa na uhakika kuwa ''kura halali'' zinapigwa,
Mpinzani mkuu wa Netanyahu Benny Gantz, ni Luteni Generali mstaafu, aliyeanzisha chama cha bluu na nyeupe mwezi Februari, akiahidi kuiunganisha nchi ambayo anadai ''imepoteza mwelekeo''.
Netanyahu anakabiliwa na mashtaka gani?
Mwishoni mwa mwezi Februari, wakili wa serikali Avichai Mandelblit alimfahamisha Bwana Netanyahu kuwa ana mpango wa kumfungulia mashtaka rasmi kuhusu shutuma za rushwa,udanganyifu na kuvunja uaminifu.
Waziri mkuu anadaiwa kupokea zawadi kutoka kwa wafanyabiashara matajiri na kutoa hongo ili aweze kupata sifa nzuri kwenye vyombo vya habari.Netanyahu amekana kufanya makosa hayo na kusema kuna njama za kisiasa dhidi yake.
Tarehe ya kusikilizwa mara ya mwisho, ambapo waziri mkuu na mawakili wake watapata muda wa kujitetea, bado haijatangazwa.Bwana Mandelblit amesema Mahakama kuu itaamua kama bwana Netanyahu aondoke madarakani au la, kwa vile anashtakiwa.
Mwanajeshi wa zamani anayejaribu kumng'oa Netanyahu
Marekani kununua mfumo wa Israel wa kujilinda dhidi ya makombora
Kumekuwa na ripoti zinazosema kuwa Netanyahu anajaribu kupenyeza hoja kwa washirika wake wa kisiasa kupitisha sheria ambayo itampa kinga ya kutoshtakiwa akiwa madarakani
Majuma ya hivi karibuni kumekua na msuguano kati ya wanamgambo wa Israel na Palestina katika ukanda wa Gaza, na Rais wa Marekani,Donald Trump anatarajiwa kutangaza mpango wake wa kutatua mzozo wa muda mrefu kati ya Israel na Palestina hivi karibuni.
Hata hivyo ,mchakato wa amani haukua jambo la kipaumbele katika mjadala wa kuelekea uchaguzi.Raia wengi wa Israeli hawana matumaini makubwa kufikia suluhu ya mzozo kati ya nchi hizo mbili.

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728