10 Julai 2016

Polisi wakanusha kuzuia mikutano ya kisiasa TZ

Jeshi la polisi nchini Tanzania limetoa ufafanuzi kuwa halijazuia mikutano ya vyama vya kisiasa
Katika taarifa yake,limesema kuwa kile lilichozuia ni mikutano ya hadhara ambayo lilihisi itavuruga hali ya usalama
Hivyobasi jeshi hilo sasa limewataka wananchi kupuuza taarifa kuwa wao walizuia mikutano ya kisiasa.
"Jeshi la Polisi linapiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara kuanzia tarehe
07/06/2016 hadi hapo hali ya kiusalama itakapotengemaa."
Kulingana na nukuu hiyo jeshi hilo linasema kuwa hakuna sehemu yoyote iliyopiga marufuku mikutano ya kiutendaji na kiutawala ya vyama vya kisiasa inayofanywa kwa mujibu wa katiba na kanuni za vyama husika.
Jeshi hilo limetoa mfano wa Chama cha CUF kilichotangaza kuwa kimepanga kufanya mkutano mkuu kujaza nafasi ya Mwenyekiti wao wa Taifa tarehe 21 Agosti, 2016,na ambao Polisi hawakujitokeza kuuzuia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728