01 Aprili 2017

Bibi wa miaka 60 kwa tuhuma za kuwachoma wajukuu wake

JESHI la Polisi mkoani Simiyu, linamshikilia mkazi wa Bariadi mkoani hapa, Joyce Mganga (60), kwa kosa la kuwachoma moto wajukuu zake kwa kutumia panga la
moto.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Jonathan Shana, alisema tukio hilo lilitokea Machi 24, saa 2 usiku, bibi huyo inadaiwa kuwa alishirikiana na mtoto wake Faraja Misano (30) kuwafanyia ukatili huo.

Kamanda Shana alisema, chanzo cha watoto hao kufanyiwa ukatili huo, ni kuwatuhumu kuwa ni wezi na kudai kuwa walimchukulia baba yao mdogo (Faraja) fedha Sh. 25,000.

Watoto waliojeruhiwa ni Neema Godrey (15), na Anastazia Misano (13) ambao walikuwa wanaishi na bibi yao kutokana na baba yao mzazi kufariki.

Hata hivyo, wakati jeshi la polisi likiendelea kumsaka kijana wa bibi huyo ambaye alitoroka, bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kumfikisha mahakamani.

Aidha, polisi imeitaka jamii kuacha tabia ya kuwafanyika watoto ukatili kwa kuwa watakaobainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao ili iwe fundisho kwa wengine.

Wakati huo huo jeshi hilo limewakamata Juma Kulwa (25), Juma Makulwa (33) na Maka Sibusa, wakazi wa kijiji cha Kadoto, wilayani Maswa kwa kosa la kumkata mapanga Mwalu Ngusa (25) kwa kumtuhumu kuwaroga watoto wa jirani yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728