18 Februari 2016

Refarii apigwa risasi na mchezaji Argentina

Refarii mmoja nchini Argentina amepigwa risasi na kuuawa na mchezaji aliyemuonesha kadi nyekundu uwanjani katika mechi ya daraja la pili.

Refarii huyo Cesar Flores alikuwa akisimamia mechi baina ya timu zinazoshiriki ligi ya daraja la chini mjini Cordoba, takriban kilomita 700 Kaskazini mwa Buenos Aires.
Polisi wameanzisha msako mkali kumtafuta mchezaji huyo ambaye hadi sasa hajatajwa.
Refarii Flores alimuonesha kadi nyekundu mchezaji huyo na akaondoka uwanjani kama ilivyo ada.
Lakini baada ya kipindi fulani alirejea akiwa amefoka uwanjani na kumfyatulia refarii huyo risasi 3 ; Kifuani, shingoni na kichwani.
Refarii huyo mwenye umri wa miaka 48 alifariki papo hapo.
Mchezaji mwenza aliyejaribu kumshawishi asimuue refarii alipata majeraha mabaya.
Hii si mara ya kwanza kwa refarii kusini mwa Marekani kushambuliwa kutokana na uamuzi wake uwanjani.
Mwaka uliopita refarii mmoja huko Brazil alilazimika kutoa bunduki ilikumzuia mchezaji mmoja asimshambulie.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728