18 Februari 2016

Kizza Besigye akamatwa na polisi Uganda


Msemaji wa chama cha Forum for Democratic Change Ssemujju Ibrahim Nganda amethibitisha kwamba mgombea urais wa chama hicho Dkt Kizza Besigye amekamatwa.

Amekamatwa akiwa eneo la Naguru, Kampala katika nyumba ambayo upinzani ulidai wizi wa kura ulikuwa ukifanyika.
Wafuasi wa upinzani, Besigye akiwemo, walitaka kukagua nyumba hiyo lakini wakazuiliwa.
Besigye alikamatwa na maafisa wa polisi walioondoka naye kutoka eneo hilo.
Haijabainika amepelekwa wapi.

Hii na mara ya pili kwa Dkt Besigye kukamatwa wiki hii.
Jumatatu, alikamatwa alipokuwa akijaribu kupitia katika barabara moja mjini Kampala.
Besigye 
Image caption Jumatatu polisi walisema walimzuilia kumlinda
Polisi walisema hakuwa na idhini ya kupitia eneo hilo kwa mujibu wa sheria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728