Jeshi la Nigeria limepiga marufuku matumizi ya farasi na punda katika jimbo la Kaskazini Mashariki la Borno
Jeshi la Nigeria
limepiga marufuku matumizi ya farasi na punda katika jimbo la Kaskazini
Mashariki la Borno, kama sehemu ya juhudi za vita dhidi ya Boko Haram .
Kundi hilo limekua likitumia farasi kutekeleza mashambulizi dhidi ya wanavijiji 
Lakini tayari kuna marufuku ya matumizi ya piki piki ambazo zilikuwa zikitumiwa na wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram kuwasafirisha wapiganaji wake katika mashambulizi.

Punda hutumiwa kwa kusafirishia bidhaa na mara nyingi farasi huendeshwa katika tamasha za kidini na kitamaduni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni