07 Januari 2015

Mwanamume mweye jinsi mbili asimulia maisha yake

BBC, Uingereza. Mwanamume mwenye jinsi mbili, amezungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na kusema kama wazazi wake wangemshauri kuhusu hali hiyo, asingeogopa kujitambulisha ulimwenguni.
Mwanamume huyo anayejitambulisha kwa jina la Triple D (25) kutoka Mashariki mwa pwani ya Marekani alisema kutokana na hali hiyo amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake 1,000, kutokana na kutodumu nao muda mrefu.
Alisema sehemu zake hizo zinafanya kazi vyema na kwamba hajabahatika kuwa na uhusiano wa kimapenzi uliodumu.
Mwanamume huyu pia anaugua ugonjwa unaoitwa ‘diphallia.’
Kwa mujibu wa Jarida la Afya la BMJ, mwanamume mmoja kati ya milioni tano, duniani huzaliwa na hali hiyo.
“Maisha yangu hayatakuwa sawa tena ikiwa nitajitambulisha duniani,” alisema Triple D. Hata hivyo, Triple D alisema BBC ilikubali kuhifadhi jina la kijana huyo na hata kutoonyesha sura yake.
Alisema hataki kuwa kichekesho kwa jamii hasa anakoishi.
Alisema alipokuwa mdogo, wazazi wake walimwambia kuwa kutokana na maumbile yake, yeye ni mtoto mwenye jinsi za kipekee.
Alisimulia kuwa wazazi wake walimkalisha chini na kuanza kumwelezea kwamba asithubutu kucheza mchezo ya kitoto na wala asivue nguo za ndani mbele ya watu.
Kutokana na mawaidha ya wazazi wake, alisema kwamba aliweza kuwa msiri, lakini alipokuwa shule ya sekondari wanafunzi wenzake waligundua na ndipo alipopata masaibu mengi.
“Mwanzoni, sikutaka wanafunzi wengine shuleni wajue hali yangu, kwa kuwa sikupenda kumuudhi yeyote,” alisema.
Triple D alisema anatamani wazazi wake wangemwambia kwamba watu wakimwona katika hali hiyo watamcheka.
“Sikutaka wanamume wenzangu kuhisi vibaya kutokana na hali niliyonayo mimi na kuanza kuniona kama mimi siyo mtu wa kawaida,” alisema Triple D.
Alisema alipokuwa na miaka 16, alitaka kufanyiwa upasuaji ili kuondolewa jinsi moja kwa sababu wasichana walikuwa wakimtazama sana katika maeneo hayo.
“Natamani sana wazazi wangu wangenishauri kuhusu hali yangu kwani nisingeogopa kujitangaza hata kidogo ,” alisema.
Triple D alisema changamoto kubwa ni kununua nguo za ndani zinazolingana na maumbile yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728