09 Januari 2015

Panya Road wafurika mahabusu Dar

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limeendelea na kamatakamata ya vijana wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu wa kutumia silaha na uporaji, walio maarufu kwa jina la Panya Road.

Watuhumiwa 329 zaidi wametiwa mbaroni jana katika operesheni iliyofanyika katika mikoa miwili ya kipolisi, Temeke na Ilala na kufanya idadi yao kufikia 953.
Operesheni hiyo inatokana na tukio la Januari 2, mwaka huu katika eneo la Magomeni Kagera ambapo vijana hao walipambana na polisi, ambapo 36 walikamatwa.
Akizungumzia operesheni hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki, alisema imefanyika maeneo mbalimbali ya mkoa wake.
Alisema maeneo ambayo vijana wengi wamekamatwa ni kwenye vijiwe vya wanaojihusisha na uvutaji bangi, dawa za kulevya na unywaji wa pombe haramu ya gongo.
“Vijana hawa hawana dhamana kwa sababu ndio chimbuko la kundi la Panya Road, wanaohatarisha amani kwa wananchi ambao wanashindwa kufanya kazi zao kwa uhuru na amani,” alisema Kamanda Nzuki.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kihenya Kihenya, alisema uchunguzi wa baadhi ya wahalifu waliokamatwa umekamilika na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.
Alisema wahalifu 68 kati ya 168, uchunguzi wao umekamilika na watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
“Wapo wengine tuliwakamata kwa bahati mbaya tumewaachia, lakini 68 uchunguzi wao umekamilika tutawafikisha mahakamani wakati waliosalia wanaendelea kuchunguzwa,” alifafanua Kamanda Kihenya.
Kutokana na kuongezeka kwa idadi kubwa ya vijana wanaofanya uhalifu huo, MTANZANIA ilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleimani Kova, kwa lengo la kujua watuhumiwa hao wamehifadhiwa wapi.
Kamanda Kova, alisema idadi ya vijana waliokamatwa ni kubwa, lakini baadhi yao uchunguzi umeshakamilika na wameshafikishwa mahakamani, wengine wanaendelea kuwahoji na taarifa nyingine ataitoa leo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728