10 Mei 2015

Tanzania mwenyeji Kagame Cup

Mabingwa watetezi wa Kagame Cup,El-Merreikh ya Sudan.
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) imekubali kuwa wenyeji wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati ngazi ya vilabu inayojulikana kama Kagame Cup.

Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ambao ndio wamiliki wa mashindano haya na hutoa mialiko kwa vilabu vyenye sifa ya kushiriki. Watatoa orodha ya vilabu shiriki na ratiba ya michuano hiyo baade mwezi huu au mapema mwezi ujao.
Afisa habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema uamuzi wa kukubali kuwa wenyeji umetolewa na shirikisho hilo mapema Jumapili baada ya kuombwa na Cecafa.
Michuano hii inatarajiwa kufanyika nchini Tanzania kuanzia tarehe 11 Julai mpaka 02 Agosti 2015.
Michuano hiyo inadhaminiwa na Raisi wa Rwanda, Paul Kagame na hufanyika kila mwaka katika nchi mwanachama za ukanda wa Afrika ya Mashariki na Kati. Rwanda ndio ilikuwa mwenyeji wa michuano ya mwaka jana inayohusisha vilabu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728