15 Aprili 2018

Raia wa Afrika Kusini watoa heshima za mwisho kwa marehemu Winnie Mandela


Raia wa Afrika Kusini wamuaga Winnie Mandela

Maelfu ya watu wamekusanyika nchini Afrika Kusini kwa mazishi ya mwanaharakati wa kampeni dhidi ya
ubaguzi wa rangi nchini humo Winnie Madikizela-Mandela.
Maelfu ya waombolezaji walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Soweto karibu na mji mkuu wa Johannesburg ambapo Winnie Mandela anazikwa.
Jeneza lake lilifunikwa na bendera ya taifa hilo na rais wa Afrika Kusini alisoma kumbukumbu ya marehemu.
Bi Madikizela Mandela , ambaye ni mke wa zamani wa Nelson Mandela alifariki mapema mwezi huu akiwa na umri wa miaka 81.



Bi Madikizila Mandela alipongezwa kwa mchango wake wakati wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi nchini Afriika Kusini.
Lakini baadaye aliipuuzwa na wanasiasa wakuu kwa kuunga mkono mauaji ya majasusi wa serikali.

Mwana wa Madikizela Mandela , Zenani Mandela Dlamini aliwashutumu wale aliotaja walikuwa na kampeni mbaya ya kumchafulia jina mamake na kumtenga kabla ya kumsafishia jina baada ya kifo chake.
''Inakera kuona vile walivyomchukulia wakati wa maisha yake, wakijua vile walivyomuumiza. Wanajua ni kwa nini waliamua kuanza kusema ukweli baada ya kifo chake'', alisema Bi Mandela Dlamini.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728