03 Aprili 2018

Mbunge awahimiza wanaume waoe wake wengi Kenya

Mbunge mmoja nchini Kenya amefufua tena mjadala wa iwapo wanaume wanafaa kuwaoa wanawake wengi.


Gathoni wa Muchomba, ambaye ni mwakilishi wa wanawake kutoka kaunti ya Kiambu, amesema wanauem wakiwaoa wanawake wengi mengi ya matatizo ya kijamii yatafikia kikomo.

Video yake akitoa wito kwa watu wa jamii ya Wakikuyu kurejelea utamaduni wa kuwaoa wake wengi imesambaa sana katika mitandao ya kijamii nchini humo.

Amedai tangu jamii hiyo ilipotupilia mbali utamaduni huo, matatizo mengi yametokea ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaorandaranda mitaani.

Mwaka 2014, Rais Uhuru Kenyatta aliidhinisha Sheria ya Ndoa ambayo inawaruhusu wanaume kuoa wanawake wengi kisheria iwapo watasajili ndoa zao kama za kitamaduni au za Kiislamu.

Wakristo hata hivyo hawaruhusiwi kuoa wake wengi chini ya sheria hiyo.

Bi Muchomba alisema wengi wa wabunge tayari wamewaoa wake wengi na “wanajivunia” jambo hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728