08 Aprili 2015

Uganda yawakamata washukiwa wa Mauaji

Uganda inasema imekamata watu kadhaa kuhusiana na mauaji ya mwendesha mashtaka Joan Kagezi yaliyotokea wiki iliyopita.
Mwendesha mashtaka huyo aliuawa na watu waliokuwa na bunduki wakitumia pikipiki na polisi kuanza uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo.
Tangu kuuawa kwa mwendesha mashtaka huyo wiki iliopita polisi imekuwa katika tafuta tafuta ya wale waliofanya kitendo hicho na hadi sasa haijaweza kupata nani anaehusika haswa,
lakini leo polisi inasema huenda imepata fununu.

Akaunt 86 za watu binafsi zafungwa Kenya

Waziri mstaafu wa mambo ya ndani wa Kenya Joseph Nkaissery, ameithibitishia BBC kwamba serikali ya Kenya imesitisha matumizi ya akaunti za watu binafsi wapatao themanini na sita wanaohusishwa na ufadhili wa kundi la kigaidi la Al Shabaab nchini humo.

07 Aprili 2015

Watu 140 wauawa Yemen katika vita vilivyopamba moto

Mapigano makali kati ya waasi wa Houthi na wapiganaji watiifu kwa utawala wa Yemen yamesababisha vifo vya watu 140 huku shirika la msalaba mwekundu likishindwa kufikisha misaada ya kibinadamu kwa waathiriwa.

Azam kutetea ubingwa Tanzania bara

Timu ya Azam imesema ina imani ya kutetea ubingwa wa Tanzania Bara ikiwa tayari kuwakaribisha wagonga nyundo kutoka jijini Mbeya, Mbeya City katika uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam Jumatano wiki hii.
Msemaji wa Azam, Jafari Idd amesema lengo ni kushinda na hatimaye kuongoza tena ligi hiyo.
Azam, iliyoanzishwa mwaka 2007, ipo nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 36 wakati wapinzani wao, Mbeya City wapo nafasi ya 7 wakiwa na pointi 24.

Kanumba Day: Jumbe Mbalimbali za Mastaa wa Bongo Movies

Kanumba Day: Jumbe Mbalimbali za Mastaa wa Bongo MoviesLeo imetimia  miaka mitatu  tangu aliekuwa staa nguli wa Bongo Movies, Steven Kanumba afariki dunia, hizi ni baadhi ya jumbe ambazo mastaa kutoka Bongo Movies wameziandika kuonyesha kumbukumbu zao kwa staa huyo.
Ni siku ambayo siwezi kusahau maisha yangu yote pumzika kwa amani kanumba wangu., nilikupenda ila mungu alikupenda zaidi . Pumzika kwa amani.
Johari
Huwezi kutaja mafanikio ya bongo movies bila kukutaja wewe...tunakuthamini na tunakukumbuka milele
JB
Steven Charles Kanumba pengo lako mpaka leo atujaweza kuliziba na sidhani kama tutaweza tena ingawa Sasa umetimiza miaka mitatu tangu ulipotuacha ghafla kiukweli ni ngumu sana kusahau Tutakukumbuka daima kwani tunapozungumzia kiwanda cha sinema nchini lazima tulitaje jina lako kaka angu ...R.I.P KANUMBA.

Lulu: Nilishalia Sana, Nishaumia Sana Lakini Kwasasa

Lulu: Nilishalia Sana, Nishaumia Sana Lakini Kwasasa…….Staa mrembo kutoka Bongo Movies Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameamua kutoboa kile alichokiita kama faraja yake kwa hivi sasa.
“Faraja YANGU...Nishalia sana,nishaumia sana lakini kwa sasa nikiona mmoja kati ya hawa analia au kuumia ndo kitu kinachoweza kuniumiza zaidi...!MUNGU awatunzeeee”-Lulu aliandika hayo jana usiku kwenye ukursa wake mtandaoni mara baada ya kuweka picha ya mama yake na mdogo wake.
Kufuatia andiko hilo komenti za mashabiki wengi zilielekea zaidi kumzungumzia kifo cha Steven Kanumba kwani leo tarehe 7  mwezi huu ni siku ya kumbukumbu cha kifo cha staa huyo wa Bongo Movies ambae alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Lulu.

Baada ya Kutemana na Mumeo,Shamsa Atoka na Nay Wa Mitego!

Baada ya Kutemana na Mumeo,Shamsa Atoka na Nay Wa Mitego!Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Shamsa Ford ambae hivi majuzi aliweka wazi kuachana na mume wake ambae wamezaanae mtoto mmoja, imebainika kuwa kwasasa yupo kwenye mahusino ya kimapenzi na Staa wa Bongo Fleva, Nay Wamitego.

Marubani wa India wazikunja kisa?

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakati dunia bado ikiwa na kumbukumbu mbaya ya ndege ya shirika la ndege la Ujerumani na vifo vya abiria 150 ndaniye,kituko kingine kimegubika tasnia ya urubani baada ya marubani wawili kuondolewa kwenye zamu ya urushaji ndege kufuatia madai ya wawili hao kuzikunja katika chumba cha kuongozea ndege.
Marubani hao hurusha ndege za shirika la ndege la India, Air India walishushwa katika ndege yao baada ya rubani msaidizi kumshambulia captain wake ama nimwite rubani kiongozi .

Liverpool must spend more to win the league, says Ray Houghton

Liverpool
Liverpool need to break their wage structure if they are to win the Premier League, according to former player Ray Houghton.
His comments come after forward Raheem Sterling rejected a new £100,000-a-week contract to stay at Anfield.

Gossip column: Van Persie, Cavani

Mirror back pageManchester United striker Robin van Persie, 31, will be sold this summer and replaced by 28-year-old Paris St-Germain forward Edinson Cavani as Red Devils boss Louis van Gaal spends £150m to overhaul his squad

Yanga kukwaana na Etoile du Sahel

Sasa ni wazi kuwa wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya vilabu ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Yanga watacheza na Etoile du Sahel ya Tunisia katika raundi ya pili ya michuano hiyo.
Yanga imefanikiwa kuwatoa Platinum FC licha ya kufungwa 1-0 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Bulawayo, nchini Zimbabwe. Hii inafuatia ushindi wa 5-1 ambao Yanga uliipata katika mechi ya kwanza iliyochezwa Dar es Salaam, Tanzania.

Man City: Manuel Pellegrini's problems & Sergio Aguero's blues

Glenn Murray scores for Palace
Manager Manuel Pellegrini says he is "not concerned" about his future, despite Manchester City's title defence being severely damaged at Crystal Palace.
A 2-1 defeat at Selhurst Park extended the champions' dismal form to four wins in 11 league games, a run which leaves them fourth, nine points behind leaders Chelsea.

Mahari ni mzigo kwa wanaume?

Mwanamume mmoja kutoka upande wa kaskazini magharibi mwa Pakistan ,amempiga risasi mpenzi wake wa zamani na watu tisa wa familia ya mwanamke huyo mwishoni mwa wiki ;hata hivyo inaelezwa kuwa mwanamume huyo miezi sita iliyopita aliwaua wazazi wake pamoja na kaka zake wawili kwa kosa la kukataa kumlipia mahari.
Kijana huyo mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 25,ambaye polisi wamemtaja kwa jina la Mir Ahmad Shah,ambaye alikuwa mafichoni baada ya kufanya shambulizi la kutumia silaha kwa kutumia bunduki aina ya AK-47 katika wilaya ya Charsadda jimbo la Khyber Pakhtunkhwa.

Makaburi yafukuliwa Tikrit

Wataalamu wa kuchunguza maiti, wameanza kuyafukua zaidi ya makaburi 12 ya halaiki, katika mji wa Tikrit, nchini Iraq.
Hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya wapiganaji wa Islamic State, kutimuliwa nje ya mji huo.
Makaburi hayo yaanaminika kuwa na zaidi ya maiti elfu moja mia saba ya wanajeshi waislamu wa Kishia, waliouwawa vibaya mwezi Juni mwaka jana na wanamgambo wa I-S.

Ugaidi:Tanzania yajiweka katika tahadhari

Waziri wa Mambo ya ndani nchini Tanzania amesema nchi hio ipo katika tahadhari ya juu kufuatia taarifa za vyombo vya habari nchini humo kwamba, kuna uwezekano wa shambilio la ugaidi katika miji ya Dar es salaam na Mwanza.

06 Aprili 2015

Picha: Mtoko wa Pasaka wa Irene Uwoya Huko Mwanza

Picha:  Mtoko wa Pasaka wa Irene Uwoya Huko MwanzaHizi ni baadhi ya picha ambazo staa mrembo Irene Uwoya ame-share nasi kupitia ukursa wake kwenye mtandao wa Instagram akiwa jijini Mwanza amabako alikwenda hivi juzi kati kikazi zaidi.
Huu ndio ulikuwa mtoko wake wa sikukuu ya PASAKA hapo jana. Mbali ya picha hizi kusababisha mafuriko ya LIKES na COMMENTS huko Instagram, Sio mbaya nawewe hapa kama mdau ukasafisha macho na picha hizi na kufunguka chochote kuhusu mtoko huu wa mrembo huyu ambae anatajwa kama ni mmoja kati waigizaji wa rembo zaidi hapa Bongo.
Kwa upande wangu Irene ndio staa alitokelezea bomba zaidi kwa siku ya jana. Umependeza sana Uwoya.

Boko Haram lawaua watu 20 Nigeria

Watu 20 wameuawa mashariki mwa Nigeria kufuatia mashambulizi mapya yanayoendeshwa na kundi la Boko Haram katika eneo hilo.
Eneo la kwaJaffa, katika jimbo la Borno, lilishambuliwa Jumapili jioni na washambulizi hao waliowashambulia wananchi na baadaye kuteketeza nyumba zao.
Majuma machache yaliyopita miji kadhaa na vijiji vilikombolewa na wanajeshi wa Nigeria wakisaidiwa na Chad, Cameroun na Niger.

Factory working conditions for women in Lesotho

Lesotho's textile industry is the biggest employer in the country.
The tiny country, which is surrounded by South Africa, relies on this industry which generates exports worth $340m a year.
But what are working conditions like for women - who make up 80% of the workforce?

Mtoto azaliwa bila pua

Eli Thompson alizaliwa tarahe nne Machi jioni, lakini alikuwa na kasoro moja, hakuwa na pua.
Siku niliyojifungua, kila kitu kilikuwa sawa.'' Mamake Brandi McGlathery ameambia ABC News Today nchini Marekani.
''Alipozaliwa daktari alimweka kifuani mwangu. Nilipomwangalia kwa karibu, nilisema ' Hana pua'. Walimchukua na kutoka naye.

Reanne Evans faces Ken Doherty in World Championship qualifying

Reanne Evans Reanne Evans will face former world champion Ken Doherty in the first round of qualifying as she bids to become the first woman to appear in the main stages of the World Championship.
Englishwoman Evans, 29, is the 10-time ladies' champion.
Doherty won the tournament in 1997, but the world number 43 has not reached the third round at the Crucible since 2006.

Wanachuo wa Garissa waombewa.

Wakristo nchini Kenya wametumia maadshimisho ya misa za sikukuu ya pasaka kote nchini humo kuwaomboleza waathirika wa mauaji ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa.
Makanisa mengi nchini humo yaliomba ulinzi wa askari wenye silaha kuwalinda wakati wa ibada .Ibada hizo zilikuwa maalumu kuwaombea marehemu wapatao mia moja na arobaini na nane waliouawa na kundi la wanamgambo wa Al Shabaab ambao waliwalenga wakristo zaidi katika shambulio hilo.

Vita vikali vyaendelea kusini mwa Yemen

Duru kutoka Yemen zasema kuwa makabiliano makali kati ya waasi wa Houthi na wanajeshi walio watiifu kwa rais wa Yemen Abd Rabbu Mansour Hadi, yanaendelea kusini mwa nchi hiyo katika mji wa Aden.
Ndege moja ya kijeshi ya Saudi Arabia imetekeleza mashambulizi makali katika ngome ya Houthi viungani mwa mji wa Aden.

Hierro says success is in Madrid's genes

A central defender and defensive midfielder of awesome ability, Fernando Hierro anchored the Real Madrid CF sides that won UEFA Champions League finals in 1998, 2000 and 2002. With Carlo Ancelotti's current side having ended a 12-year wait by winning La Décima last season, the 47-year-old recalled his team's golden years and predicted that this could be the start of a similarly glorious spell for the club.

Mwigizaji Jack Wolper Ashutumiwa Kumsahau Aliyemtoa Kisanii Katika Tasnia ya Filamu Bongo

Mwigizaji Jack Wolper Ashutumiwa Kumsahau Aliyemtoa Kisanii Katika Tasnia ya Filamu BongoUbuyu Mpya Kutoka Instagram kwenye page ya mrekebishatabia kuhusu Mrembo Mwigizaji Wolper Kumsahau aliyemwingiza katika Tasnia ya Filamu:

'HISTORIA: Je unajua aliyemtoa kisanii Jackline Wolper mpaka kupata umaarufu nchini ni nani? Ni mdada mkali wa wa siku nyingi kwenye masuala ya sana Lucy Komba ambaye hivi sasa anaishi na familia yake nchini Denmark.

Conor McGregor: UFC fighter ready for world title showdown

Conor McGregor fighting Max Holloway in August 2013 Conor McGregor has fought just five times in the Ultimate Fighting Championship (UFC) but has quickly become one of the most feared sportsmen on the planet.
The mixed martial artist from the Republic of Ireland possesses a devastating knockout punch in both hands.
And if his left or his right doesn't finish an opponent, the man nicknamed 'The Notorious' will carve out a unanimous decision with pin-point precisions and devastating accuracy.

Lulu Atoa fundisho Kwa Shabiki

Lulu Atoa fundisho Kwa Shabiki…Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa juzikati aliamua kumjibu shabiki mmoja mtandaoni kutokana na kuwepo kwa watu wengi wanaomsema vibaya mitandaoni.
Akizungumza na mwanahabari wa GPL mara baada ya kumjibu shabiki Gladmarry Edwine aliyemkejeli kupitia mtandao wa Instagram kuwa ikifika siku ya Kanumba Day (Aprili 7, mwaka huu), Lulu atajiliza ndipo staa huyo alipomtolea uvivu iwe fundisho.
“Yule alinikuta siku hiyo siko vizuri halafu niko Instagram nikaamua kumtolea uvivu kwa kumpaka maneno ya shombo iwe fundisho,” alisema Lulu.

Bozi: Nay wa Mitego Ana Laana Yangu

Bozi: Nay wa Mitego Ana Laana YanguStaa mrembo wa Bongo Movies, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ amesema kuwa migogoro yote inayomtokea aliyewahi kuwa mwandani wake, Emmanuel Elibariki ‘Nay’ ni kutokana na laana ya kumsambazia picha zake za utupu.
Akipiga stori na paparazi wa GPL, Bozi alisema tatizo kubwa lililomkuta Nay kwa mpenzi wake Siwema kumfumania na njemba ni malipo ya kupuuza penzi lake na dhambi kubwa aliyomtendea ya kusambaza picha zake za utupu alizomtumia wakati walipokuwa kwenye uhusiano.

Shambulizi Garissa:Serikali yajitetea

Serikali ya Kenya imeitetea idara yake ya usalama kufuatia shutma kwamba ilichelewa kukabiliana na shambulio la chuo kikuu cha Garissa ambapo takriban watu 150 waliuawa.
Shambulio hilo lilisitishwa baada wapiganaji wanne waliohusika kuuawa na maafisa wa polisi saa 15 baada ya kuvamia chuo hicho.

Mahmoud Abbas kuishtaki Israel

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amekataa kukubali mamilioni ya dola ambazo ni fedha za kodi ambazo zilikuwa zimezuiliwa na Israeli.
Bwana Abbas alisema kuwa aliamua kurudisha pesa hizo kwa sababu Israeli ilikuwa imekata kiasi fulani ili kulipa kile ilichosema kuwa ni madeni kwa makampuni ya nchi yake.

Garissa:Wanafunzi kuondoa vitu vyao

Wanafunzi katika chuo kikuu cha Garissa nchini Kenya wanatarajiwa kupelekwa chuoni humo ili kundoa vitu vyao kabla ya kupelekwa nyumbani.
Serikali ya Kenya imefunga chuo hicho kufuatia shambulio la siku ya alhamisi ambapo watu 150 waliuawa.

Akon awajibu wanamuziki wa Kenya

Mwanamuziki mwenye tuzo la kimataifa Akon amesema kuwa hakuna hata mwanamuziki mmoja wa Kenya ambaye amemuomba kufanya naye 'kolabo'mara zote tano ambazo ameweza kuzuru Kenya.

Jeshi la Kenya lafanya shambulio Somalia

Ndege za kijeshi za Kenya zimeshambulia maeneo ya wapiganaji wa kundi la Alshabaab katika taifa jirani la Somalia ,msemaji wa jeshi ameiambia BBC.
Ndege hizo zililenga maeneo mawili ya jimbo la Gedo,linalotumiwa na wapiganaji hao kuvuka na kuingia Kenya, msemaji huyo ameongeza.
Maeneo hayo mawili hutumiwa na wapiganaji hao kupanga mshambulizi nchini Kenya.

Mtu anayejigamba kuwa 'mungu' Kenya

Je, umewahi kusikia mtu anajiita Mungu na ni binadamu wa kawaida na wafuasi wake wanaamini kuwa yeye ndiye muumba wao? Yuko magharibi mwa Kenya anajiita Jehova Wanyonyi na anadai kuwa yeye ndiye Mungu

05 Aprili 2015

Wajivunia kuwa makahaba Australia

Hivi umeshawahi kujiuliza kwamba wafanyabiashara ya ngono ni watu wa namna gani? Ama biashara hiyo ni biashara kama biashara zingine kivipi? Nchini Australia,maelfu ya wafanyabiashara ya ngono bila soni wameweka bayana namna wanavyotumia mitandao ya kijamii na kuueleza ulimwengu jinsi wanavyo fanikisha biashara hiyo.
Huwa hawachagui wateja,Mwanafunzi mwenzangu? Mwanasheria nimtakaye,mwanaharakati,binti yangu?dada yangu, mfanya biashara mwenzangu wa ngono? Familia yangu! Sihitaji msaada wao.

Garissa:Redio 2 zafungwa Somalia.

Mamlaka nchini Somalia imevifunga vituo viwili vya redio nchini humo baada ya kutangaza habari za wapiganaji wa Al-shabaab kuhusu shambulio la chuo kikuu nchini Kenya.
Kituo cha redio cha Sky FM na kile cha Shebelle vilifungwa huku mtangazaji na mkurugenzi wakikamatwa.
Vikosi vya usalama nchini Somali vimekuwa vikiwakamata wanahabari ambao hufanya mahojiano na wapiganaji wa Al-shabaab ama kutangaza habari zao.

03 Aprili 2015

Filamu Zakiasili za Mpa Dili Husna

Filamu Zakiasili za Mpa Dili HusnaStaa mrembo wa filamu, Husna Chobis amefunguka kwa kusema kuwa filamu alizoigiza za kiasili zimepata dili la kwenda kuigiza nchini Uingereza, baada ya kuchaguliwa kupitia sinema ya Gawa na Ndase alizoigiza na kumpatia umaarufu.
“Namshumkru Mwenyezimungu kwa kuonyesha kipaji changu uigizaji na hasa filamu za asili, najua wazi kama si filamu hizi isingekuwa rahisi kuchaguliwa na kuja hapa Uingereza kushiriki filamu ninayocheza sasa, filamu za asili zimenipa dili,”anasema Husna.
Msanii huyo yupo nchini uingereza pamoja wasanii wenzake wawili yaani Eshe Buheti na Yusuf Mlela zaidi ya mwezi mmoja wakirekodi filamu inayoshiriki raia wa Afrika ya Mashariki na wasanii kutoa Afrika Magharibi nchi za Naijeria na Ghana.

HUU NI UNYAMA ULIOKITHIRI HUKO KENYA

Mungu atusaidie

Liverpool yamng'ang'ania Raheem Sterling

Kocha wa Liverpool ya England Brendan Rodgers, amesema Raheem Sterling hataondoka katika klabu hiyo, msimu wa kiangazi japo kuwa mazungumzo kuhusu mpango mpya kati ya mchezaji huyo na vijogoo hao wa Anfield yamevunjika.

Ugaidi:Rais wa Somalia ataka ushirikiano

Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, amesema kuwa Somalia na Kenya zinafaa kuimarisha uhusiano wao dhidi ya ugaidi, baada ya wapiganaji wa kiislamu kushambulio chuo kimoja kikuu mjini Garrisa hapo jana Alhamisi.
Watu 147 waliuwawa wengi wao wakristo, baada ya wanamgambo hao wa Al- Shaabab kutumia kigezo cha kidini ili kuwatenganisha.

Ray Atoboa ya Moyoni Kuhusu Filamu ya OPRAH

Ray Atoboa ya Moyoni Kuhusu Filamu ya OPRAHNi kati ya movie ninazozipenda sana . pia naweza thubutu kusema ni movie iliyofanya mabadiliko makubwa sana kwenye film industry nchini kwetu Tanzania na nje ya mipaka yetu. pia ndiyo movie iliyomtangaza Irene Uwoya kwenye ulimwengu wa filamu. kwa hiyo nina kila sababu ya kuipenda movie hii. OPRAH HOT SUNDAY”. Ray ameandika kwenye ukurasa wake wa mtandaoni mara baada ya kuweka picha ya kasha la filamu hiyo.
Wewe kama mdau unamaoni gani juu ya kazi hii ya OPRAH iliyotoboa mipaka ya nchi? Hebu funguka uliionaje, kama bado nakuomba itafute kwani ni moja kati ya filamu bomba kutoka Bongo Movies.

Ushindi wa Buhari ni wa kihistoria Nigeria

Ushindi wa Buhari unaadhimisha wakati muhimu katika historia ya Nigeria iliojawa na misukosuko.

Mtu mwenye umri mkubwa duniani afariki

Mtu aliyekuwa na umri mkubwa duniani kutoka nchini Japan amefariki wiki kadhaa baada ya kusherehekea miaka 117 tangu azaliwe.

Wema Akataa Unafiki, Ampongeza Diamond

Wema Akataa Unafiki, Ampongeza DiamondStaa mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Sepetu amefunguka kwa mara ya kwanza na kusema kuwa hata yeye anampa pongezi mpenzi wake wa zamani, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa jitihada alizozifanya mpaka kufikia hatua ya kumaliza nyumba yake iliyopo Madale jijini Dar.

EPL kuendea kutimua vumbi kesho

Ligi ya England itaendelea tena kesho kwa nyasi za viwanja saba kuwaka moto katika michezo ya mzunguko wa raundi ya 26.
Vinara wa ligi Chelsea watakua katika uwanja wao wa nyumbani Stamford Bridge kuwakabili Burnley walioko nafasi ya pili toka mkiani Mwa msimo wa ligi.

Kasi ya kujiunga na ugaidi yaongezeka

Zaidi ya wapiganaji wa kigeni elfu ishirini na watano kutoka mataifa mia moja walisafiri kwa nia na malengo ya kujiunga na makundi ya kijeshi kama al-Qaeda na Islamic State (IS), taarifa ya umoja wa mataifa imeeleza hayo.

Ubaguzi wa rangi wamtisha Chris Ramsey

Meneja wa timu ya QPR Chris Ramsey amesema asili yake ya rangi nyeusi itampa wakati mgumu kupata kazi pale atakapo ondoka katika dimba la Loftus Road.

Kura ya maoni yaahirishwa Tanzania

Tume ya Uchaguzi wa taifa la Tanzania, kukabiliwa na msisitizo wa muda mrefu wa wananchi juu ya kuahirishwa kwa tarehe ya kufanyika kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekzwa na tume hiyo kutoa msimamo kwamba tarehe haitobadilika, leo hii tume hiyo imetoa kauli tofauti. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi , Jaji Mstaafu Damian Lubuva ametangaza kuwa zoezi hilo la kura ya maoni limeahirishwa, jambo ambalo limezua hisia tofauti nchini Tanzanika.

Meli ya uvuvi ya Urusi yazama

Boti ya uvuvi ya Urusi imezama katika visiwa vya Kamchatka , ikiwa na mabaharia wapatao hamsini na wanne ambao inadhaniwa kuwa wamekufa maji wote.

Mazungumzo ya nyuklia ya Iran yaafikiwa

Makubaliano kuhusu muundo wa baadaye wa mpango wa nyuklia wa Iran, yamefikiwa baada ya mazungumzo na mataifa sita makubwa yaliyokuwa yakifanyika nchini Uswisi.
Mawaziri wa mambo ya naje wa mataifa sita makubwa duniani pamoja na Iran wakijadili mpango wa nyuklia wa Iran mjini Lausanne, Uswisi
Kwa mujibu wa mkataba huo, Iran itapunguza uwezo wake wa kurutubisha madini ya urani huku ikiahidiwa kuondolewa vikwazo kwa awamu.

Al Shababaab wavamia Chuo kikuu cha Garrisa Kenya

Garissa, Kenya: Masked gunmen attack Garissa University College, heavy gunfire reported in the institution as police and military engage attackers; scores injured.

02 Aprili 2015

Kanisa Katoliki linautazamaje ushoga?

Kadinali Raymond Burke mwenye asili ya Marekani ameenguliwa na Papa Francis katika wadhifa wake wa mwenyekiti wa bodi katika kanisa katoliki,ametoa onyo kwamba kuna viashiria vya kanisa hilo kuupigia chapuo ushoga, kauli hii Burke aliiotoa wakati alipokuwa akihojiwa na tovuti moja ya Italy ya La Nuova Bussola Quotidiana mara baada tu ya kuenguliwa kwenye wadhifa wake.
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728