
Wataalamu wa kuchunguza maiti, wameanza kuyafukua zaidi ya makaburi 12 ya halaiki, katika mji wa Tikrit, nchini Iraq.
Hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya wapiganaji wa Islamic State, kutimuliwa nje ya mji huo.
Makaburi
hayo yaanaminika kuwa na zaidi ya maiti elfu moja mia saba ya wanajeshi
waislamu wa Kishia, waliouwawa vibaya mwezi Juni mwaka jana na
wanamgambo wa I-S.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni