Viongozi wa vyama vya upinzani, fursa hizo mnaongezewa kuwafikishia ujumbe wananchi. Mshindwe tu wenyewe kuufikisha ujumbe huo kwa wenye nchi, halafu msiwageuke wananchi na kuanza kuwalaumu kama ujumbe wenu hauwafikii ipasavyo.
Watanzania sio wapumbavu wala sio wajinga. Mwalimu Nyerere alipozunguka nchi nzima kutafuta uhuru walimuelewa vizuri sana na matokeo yake yalionekana.
Nyinyi pia nendeni kwa wananchi hao hao, waelezeni yote upungufu uliopo waelewe. Wao pekee ndiyo wenye uamuzi wa mwisho. Tumieni fursa hizi vizuri kuwaelimisha wananchi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni