23 Novemba 2014

Ugonjwa wa tauni wawaua 40 Madagascar

Mlipuko wa ugonjwa wa tauni nchini Madagascar umewaua watu 40 na kuwaathiri takriban wengine 80 ,shirika la afya duniani WHO limesema.

WHO limeonya kuhusu hatari za kuenea kwa harahaka ugonjwa huo katika mji mkuu wa Antananarivo.
Hali inaendelea kuwa mbaya kutokana na funza wasiosikia dawa, WHO limeonya.
Binaadamu huambukizwa ugonjwa huo baada ya kuumwa na funza wanaobebwa na panya.
Iwapo ugonjwa huo utajulikana mapema basi huweza kutibiwa kwa haraka.
Lakini asilimia 2 ya visa vya ugonjwa huo nchini Madagascar ni ule hatari unaombukiza mapafu na unaweza kuenezwa kupitia kukohoa.
Kisa cha kwanza cha mlipuko wa ugonjwa huo kilijulikana katika kijiji cha Soamahtamana wilayani Tsiroanomandidy takriban kilomita 200 magharibi mwa Antananarivo mwishoni mwa mwezi Agosti.
Kumekuwa na visa viwili vilivyothibitishwa katika mji mkuu ikiwemo kifo kimoja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728