10 Novemba 2014

Kikwere afanyiwa upasuaji marekani

Dar es Salaam. Rais, Jakaya Kikwete amefanyiwa upasuaji wa tezi dume (prostate) katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Salva Rweyemamu kwa vyombo vya habari jana imesema Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo juzi alfajiri baada ya madaktari waliomfanyia uchunguzi wa afya yake kujiridhisha kuwa alikuwa anahitaji matibabu ya aina hiyo.
“Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha saa moja unusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa,” ilisema taarifa hiyo na kubainisha kuwa hali ya Rais Kikwete inaendelea vizuri na bado yuko wodini akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba.
Taarifa hiyo iliyoambatana na picha mbili moja ikimwonyesha Rais Kikwete akiwa anazungumza na daktari bingwa wa upasuaji katika hospitali hiyo, Dk Edward  na nyingine akiwa ameketi pamoja na daktari huyo pamoja na daktari wake, Profesa Mohamed Janabi ilisema wananchi wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.
Wiki iliyopita, Kurugenzi hiyo ya mawasiliano Ikulu ilitoa taarifa za safari ya Rais Kikwete kwenda Marekani kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake na kuwa angekaa huko kwa siku 10.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728