03 Aprili 2015

Liverpool yamng'ang'ania Raheem Sterling

Kocha wa Liverpool ya England Brendan Rodgers, amesema Raheem Sterling hataondoka katika klabu hiyo, msimu wa kiangazi japo kuwa mazungumzo kuhusu mpango mpya kati ya mchezaji huyo na vijogoo hao wa Anfield yamevunjika.

Sterling mwenye umri wa miaka 20 aliiambia BBC kuwa yeye anavutiwa zaidi kutwaa mataji na wala siyo pesa,maneno ya mchezaji huyo yanakuja baada ya kukataa ushawishi wa mkataba wa kitita cha paundi laki 100,000 kwa wiki. “Liverpool ni moja ya vilabu vyenye nguvu katika soka na kama wamiliki hawataki kuuza mchezaji, hawawezi kufanya hivyo” alisema Rodgers.
Raheem Sterling
Raheem amebakiza miaka miwili katika mkataba wake wa awali ambao unamlipa kiasi cha paundi 35,000 kwa wiki.
“ Ni kweli mkazo unapaswa kuwa kwenye soka. Kama matarajio yake ni kushinda mataji ni jambo ambalo linafungamana na kile tunachokifanya sisi” aliongeza Rodgers.
Kocha huyo pia alisema kuwa Liverpool haikumruhusu Sterling kuzungumza na BBC jambo analofikiri ni makosa kufanya mahojiano. ‘‘ atajifunza sisi sote tunafanya makosa katika maisha, haswa tunapokuwa wadogo” alimalizia Brendan.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728