09 Aprili 2015

Bei za vyakula zapaa, mfumuko wa bei mwezi Machi wafikia asilimia 4.2

Dar es Salaam. Upungufu  wa chakula kwa baadhi ya mikoa nchini umeendelea kusababisha ongezeko la mfumuko wa bei wa Taifa kutoka asilimia 4.2 hadi asilimia 4.2 ndani ya mwezi mmoja.
Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Ephraimu Kwesigabo, aliwaambia waandishi wa habari leo kuwa, kutokana na upungufu huo bei za bidhaa za vyakula zimeongezeka.
“Mfumuko wa bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka unapimwa kwa kiwango cha badiliko la kasi ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi,”alisema.
Aliongeza: “Hivyo kutokana na ongezeko la bei za bidhaa hizo pamoja na huduma zote kwa kaya zimesababisha mfumuko wa bei wa taifa,”alisema Kwesigabo.
Aliendelea kueleza kuwa, kasi ya upandaji wa bei za bidhaa hizo zimesababisha mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi iliyopita kuongezeka hadi ukufikia asilimia 4.3 kutoka asilimia 4.2 ya mwezi Februari mwaka huu.
Kwesigabo alisema, ongezeko la mfumuko wa bei kwa mwezi Machi umesababishwa hasa na kuongezeka bei za bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia Machi mwaka huu tofauti na ilivyokuwa kwa Machi mwaka jana.
Alizitaja bidhaa hizo kuwa ni pamoja na mchele, unga wa muhogo, nyama, samaki, maharage, choroko na sukari.
Alisema kutokana na hali hiyo wananchi wataendelea kushuhudia bei za vyakula zikiendelea kupanda na kwamba bei waliyokuwa wakinunua bidhaa za vyakula hapo awali itabadilika.
Akizungumzia thamani ya shilingi ya Tanzania kwa mwezi uliopita ikilinganishwa na mwezi Septemba, 2010 alisema, uwezo wa Sh 100 katika kununua bidhaa na huduma umefikia Sh 64 na senti 15 mwezi Machi mwaka huu kutoka Septemba, 2010.
“…ikilinganishwa na Sh 64 na senti 59 ilivyokuwa Febriari mwaka huu,”alisema Kwesigabo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728