20 Aprili 2015

Pembe za Ndovu zanaswa Thailand

Maafisa wakuu wa idara ya forodha nchini Thailand, wanasema kuwa wamenasa shehena kubwa zaidi ya pembe za ndovu kuwahi kunaswa katika historia ya taifa hilo.

Wanasema kuwa wamefuatilia chimbuko la shehena hiyo yenye uzito wa tani nne ya pembe za ndovu na kubaini zilitoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Maafisa hao wanasema kuwa pembe hiyo inayogharimu dola milioni sita ilikuwa njiani kwenda mjini Laos, ambako inaaminika ingeuzwa kwa wateja nchini Thailand, China au Vietnam.
Thailand inakabiliwa na vikwazo vya kiuchumi kuhusu namna inavyozembea katika kukabiliana na bidhaa za wanyama pori zinazouzwa nje ya Nchi hiyo, iwapo haitafanya lolote kuzuia biashara hiyo haramu ya pembe za ndovu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728