07 Aprili 2015

Yanga kukwaana na Etoile du Sahel

Sasa ni wazi kuwa wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya vilabu ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Yanga watacheza na Etoile du Sahel ya Tunisia katika raundi ya pili ya michuano hiyo.
Yanga imefanikiwa kuwatoa Platinum FC licha ya kufungwa 1-0 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Bulawayo, nchini Zimbabwe. Hii inafuatia ushindi wa 5-1 ambao Yanga uliipata katika mechi ya kwanza iliyochezwa Dar es Salaam, Tanzania.

Vigogo hao wa Tunisia, wenye uzoefu wa kucheza michuano mikubwa Afrika, imepata nafasi ya kucheza na Yanga baada ya kutoka sare ya 1-1 na timu ya Benfica de Luanda. Katika mechi ya kwanza, Watunisia walishinda 1-0.
Kocha wa Yanga, Mdachi Hans Pluijm atakuwa na kibarua cha ziada kuwahkikisha wanasonga mbele huku nahodha wake, Nadir Haroub “Cannavaro” akisema wapo tayari kucheza na timu yoyote katika michuano hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728