08 Septemba 2015

Je umeambukizwa Nomophobia? Soma utafiti

Je umeambukizwa Nomophobia ?
Utafiti wa hivi karibuni uliowachunguza wanafunzi 1000 Korea Kusini umebaini kuwa asilimia 72 ya watoto wanapata simu wakifikia umri wa miaka 11 au 12.

Aidha kwa Wanafunzi hao huzitumia simu hizo za kisasa kwa karibu saa tano na nusu ya muda wao kwa siku.
Matokeo yake ni kuwa asilimia 25 ya watoto ama mmoja kati ya wanafunzi 4 ametajwa kuwa na uraibu wa simu hizo.
Simu za kisasa za mkononi katika kamataifa ya Asia zimekua kama ibaada.
Kwa mfano, nchini Japan, kuna desturi maalum ya simu za mkononi inayojulikana kama Keitai;Wanatumia simu za mikononi za kisasa kutumiana picha za chakula na vitu mbalimbali.
Lakini utumizi huu wa simu za mkononi kwa kiasi cha kupindukia umewapata baadhi yao katika mazingira yasiyo ya kawaida.
Simu za kisasa za mkononi katika kamataifa ya Asia zimekua kama ibaada.
Mkoani Sichuan, iliwabidi wazima moto kuitwa baada ya mwanamke mmoja kutumbukia ndani ya bwawa la maji taka, wakati akiwasiliana kwenye simu yake.
Mtalii mmoja raia wa Taiwan naye nusura atumbukia baharini, kisa na maana , simu.
Yamkini alikuwa akichapisha ujumbe na wenzake kiasi kuwa haoni anakokwenda.
Nomophobia
Nchi ya Singapore karibu kila raia anamiliki simu ya kisasa ya mkononi, raia huko ni milioni sita pekee.
Kwa sababu ya uraibu huu nchi imejenga kiliniki maalum ya kuwashugulikia walio na tatizo la Nomophobia, yaani kuipenda simu kupindukia.
Mmoja anayepitia matibabu ya kuugua kwa kuikosa simu ni kijana wa miaka 19 wa Korea Kusini, Emma Yoon.
Amekua na tatizo hili tangu mwaka wa 2013.
Anasema akikosa simu hasa kuisahau, moyo wake unaanza kupiga kwa kasi, anatokwa na kijasho, na hawezi kufikiria hadi aipate simu.
Anasema akikosa simu hasa kuisahau, moyo wake unaanza kupiga kwa kasi, anatokwa na kijasho, na hawezi kufikiria hadi aipate simu.
Imekua ni kama mmoja ya viungo vyake.
Wazazi wake wanasema penzi la simu alilonalo mwanao limeathiri maisha yake ikiwemo kushindwa kwenda shuleni wakati mwingine.
Lakini hofu sasa ni kwa watoto wachanga ambao pia nao wamejipata kwenye uraibu huu.
Anasema akikosa simu hasa kuisahau, moyo wake unaanza kupiga kwa kasi, anatokwa na kijasho, na hawezi kufikiria hadi aipate simu.
Utawaona watoto wa miaka 10 wakishindwa kucheza na wenzao eti kwa sababu hana simu ya kuchat,,,
Simu siku hizi bara Asia inatumika kufanya kazi ya ziada miongoni mwa wanafunzi ama ukipenda Homework.
Ndio maana hata China wamefungua kiliniki yao ya kutibu Nomophobia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728