08 Septemba 2015

Mpango wa kutega mabomu watibuliwa Kenya

Polisi wa Kenya walipokuwa wakipambana magaidi katika Chuo Kikuu cha Garisa 

 
Wanaume watatu wamakamatwa mjini Nairobi nchini Kenya baada ya mtu mmoja kuzuiwa wakati anajaribu kuingia katika jengo la maduka akiwa na kifaa cha kilipuzi katika mkoba wake.
Kifaa hiko kiliharibiwa na polisi wa kitengo cha kutegua mabomu nchini kenya.
Shuhuda anasema watu hao watatu walisimamishwa na walinzi wa usalama wakiwa wanajaribu kuingia katika jengo moja la maduka la Garden city Mall kwenye kitongoji kimoja Nairobi.
Mmoja wa wanaume hao alikataa kukaguliwa hivyo ilibidi walinzi wamdhibiti wa kumpiga ngumi.
Milipuko iligunduliwa katika mkoba wake.
Wateja na wafanyakazi wa maduka hayo waliondolewa na kifaa hicho kiliharibiwa na kitengo maalum cha kudhibiti mabomu.
Polisi anasema wanaume wote watatu wanaoshukiwa kuwa ni raia wa Kenya wamekamatwa.
Inaaminiwa kuwa bomu hilo ni kilipuzi kidogo chenye betri na kilichounganishwa kwenye simu ya mkonon ambayo ingetumia kulipua bomu hilo.
Miaka miwili iliyopita watu 67 waliuawa baada ya wanamgambo wa Al Shabaab kuvamia maduka ya Wastegate mjini Nairobi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728