08 Septemba 2015

50 Cent anajenga Kasri Afrika

 
50 Cent anajenga Kasri Afrika 
 
Rapa wa Marekani 50 Cent amechapisha picha ya nyumba yake mpya iliyoko barani Afrika katika mitandao wa kijamii ya instragram.

Picha hiyo imezua mjadala hususan baada mwanamuziki huyo nguli wa kizazi cha kufoka, kuwasilisha ombi mahakamani akidai amefilisika.
Katika ujumbe wake huo 50 cent amesema kuwa yu karibu kukamilisha ujenzi wa nyumba yake akiahidi kuandaa dhifa la kukata na shoka kwaajili ya ufunguzi wa jumba hilo.
Mwezi Julai alishtakiwa kwa kosa la kutomlipa dola milioni tano za Marekani $5m mwanamke mmoja ambaye alichapisha kanda yake ya video ya ngono katika mtandao wa intaneti.
Mwimbaji huyo wa muziki wa kufoka hakufafanua ni wapi nyumba yake ilipo lakini amesema anaishi maisha mazuri.
50 Cent anajenga Kasri Afrika
Video hiyo ilionyesha watu wakifanya kazi kando ya nyumba hiyo.
Rapa huyo anayejulikana kama Curtis James Jackson III alisema kuwa alipokuwa akisema amefilisika ilikuwa njia tu ya kujilinda kibiashara.
Yamkini 50 Cent ni mfanyibiashara wa haiba ya juu mwenye hisa na usemi katika makampuni kadhaa yanayoshughulika na mavazi,vinywaji , dondi na uchimbaji madini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728