08 Septemba 2015

Punda na farasi ni marufuku Nigeria

Jeshi la Nigeria limepiga marufuku matumizi ya farasi na punda katika jimbo la Kaskazini Mashariki la Borno

Jeshi la Nigeria limepiga marufuku matumizi ya farasi na punda katika jimbo la Kaskazini Mashariki la Borno, kama sehemu ya juhudi za vita dhidi ya Boko Haram .
Kundi hilo limekua likitumia farasi kutekeleza mashambulizi dhidi ya wanavijiji
Jimbo la Borno ndio kitovu cha vuguvugu la Boko Haram
Huku jeshi la Nigeria likionekana kupata mafanikio katika vita vyake dhidi ya Boko Haram, kundi hilo linaripotiwa kukabiliwa na kibarua kigumu kupata mafuta ya kuweka kwenye magari yake kwa hivyo hutumia farasi kwa usafiri mbadala.
Lakini tayari kuna marufuku ya matumizi ya piki piki ambazo zilikuwa zikitumiwa na wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram kuwasafirisha wapiganaji wake katika mashambulizi.
Kufuatia upungufu wa Mafuta Boko Haram imekuwa ikitumia punda na farasi kufanya mashambulizi yake
Pikipiki hizo zilirahisisha kutoroka kwa washambulizi , kwa hivyo kwa sasa kuna hofu kwamba marufuku ya sasa itadhoofisha zaidi uchumi wa maeneo ya vijijini na kuathiri maisha ya watu wa kawaida.
Punda hutumiwa kwa kusafirishia bidhaa na mara nyingi farasi huendeshwa katika tamasha za kidini na kitamaduni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728