14 Aprili 2015

Mahakama yazima vinu vya nyuklia Japan

Mahakama moja nchini Japan imetoa agizo la kuzuia kufunguliwa upya kwa kiwanda kimoja cha nyuklia iliyoko pwani ya Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Vinu 50 vya nyuklia vya
Japan vilifungwa mwaka wa 2011 kufuatia mkasa wa Fukushima.
Lakini serikali ya waziri mkuu Sinzo Abe, inashinikiza vinu hivyo kufunguliwa.
Agizo hilo lililotolewa katika mahakama ya wilaya wa Fukui, ni pigo kubwa kwa juhudi hizo za serikali.
Serikali ya waziri mkuu Sinzo Abe, inashinikiza vinu hivyo kufunguliwa ilikuimarisha uzalishaji wa kawi
Miezi miwili iliyopita mdhibiti wa nyuklia nchini humo alitoa idhini kwa mradi huo wa Takahama ulioko Kaskazini Magharibi mwa Japan kuanzisha upya uzalishaji wa kawi ya nyuklia katika viwanda vyake viwili.
Alisema kuwa mradi huo ulikuwa umetimiza masharti yote ya kiusalama na utaratibu yaliyowekwa punde baada ya mkasa wa Fukushima miaka minne iliyopita.
Lakini leo majaji katika mahakama ya Fukui wameonekana kutokubaliana na uamuzi wa mdhibiti huyo.
Badala yake wamekubaliana na kundi la wakazi wa eneo hilo waliotaka kusitishwa kwa shughuli za uzalishaji kawi katika kiwanda hicho.
Walidai kuwa kiwanda hicho hakitaweza kuhimili tetemeko kubwa la ardhi kama lile lililosababisha mkasa wa Fukushima.
Kampuni ambayo inamiliki kiwanda hicho, Kansai Electric, tayari imesema itakata rufaa dhidi ya uamuzi huo, lakini huenda utaratibu huo ukachukua miezi kadhaa au hata miaka kabla ya uamuzi kutolewa upya.
Na huenda hatua kama hiyo ikachochea wakazi wanaoishi karibu na viwanda vingine vilivyofungwa wakawasilisha kesi kama hii mahakamani.
Muungano wa waenyeji wa Fukushima hawataki vinu hivyo kuwashwa upya
Akizungumza nje ya mahakama, wakili wa kundi la watu waliowasilisha kesi mahakamani Yuichi Kaido alisema ana matumaini kuwa uamuzi huu ndio mwanzo wa kusitishwa kwa uzalishaji wa kawi ya nyuklia nchini Japan.
''Tunahitaji kuambiwa ukweli wa mambo kuhusu mkasa wa Fukushima na tunahimiza kwamba viwanda vyote vinavyozalisha kawi ya nyuklia vifungwe sio tu kiwanda cha Takahama pekee yake,"alisema Kaido
Mwanaharakati anayepinga matumizi ya nguvu za nyuklia Tadashi Matsuda aliwashukuru waathirika wa mkasa huu kwa mchango wao katika kesi hiyo.
"Huu ni uamuzi uliofanyika, kutokana na msukumo wenu kama waathirika wa mkasa huu''.
Serikali ya waziri mkuu Sinzo Abe, inashinikiza vinu hivyo kufunguliwa ilikuimarisha uzalishaji wa kawi
''Kwa wale ambao baada wanateseka huko Fukushima, Natumai habari hii itawafikia na tafadhali sikiliza haya yote yamewezekana tu kwa ajili ya mchango wako"alisema Matsuda.
Uamuzi huu ni pigo kubwa kwa serikali ya Japan ambayo inalenga kufufua sekta yake ya nyuklia.
Hadi sasa viwanda 48 vya kuzalisha nyuklia nchini humo vimefungwa kufuatia mkasa huo wa mwaka 2011.
Hata hivyo waziri mkuu wa Japan Yoshihide Suga, amesema serikali bado inamatumaini ya kufufua tena viwanda hivyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728