Japan vilifungwa mwaka wa 2011 kufuatia mkasa wa Fukushima.
Lakini serikali ya waziri mkuu Sinzo Abe, inashinikiza vinu hivyo kufunguliwa.
Agizo hilo lililotolewa katika mahakama ya wilaya wa Fukui, ni pigo kubwa kwa juhudi hizo za serikali.
Alisema kuwa mradi huo ulikuwa umetimiza masharti yote ya kiusalama na utaratibu yaliyowekwa punde baada ya mkasa wa Fukushima miaka minne iliyopita.
Lakini leo majaji katika mahakama ya Fukui wameonekana kutokubaliana na uamuzi wa mdhibiti huyo.
Badala yake wamekubaliana na kundi la wakazi wa eneo hilo waliotaka kusitishwa kwa shughuli za uzalishaji kawi katika kiwanda hicho.
Walidai kuwa kiwanda hicho hakitaweza kuhimili tetemeko kubwa la ardhi kama lile lililosababisha mkasa wa Fukushima.
Kampuni ambayo inamiliki kiwanda hicho, Kansai Electric, tayari imesema itakata rufaa dhidi ya uamuzi huo, lakini huenda utaratibu huo ukachukua miezi kadhaa au hata miaka kabla ya uamuzi kutolewa upya.
Na huenda hatua kama hiyo ikachochea wakazi wanaoishi karibu na viwanda vingine vilivyofungwa wakawasilisha kesi kama hii mahakamani.
''Tunahitaji kuambiwa ukweli wa mambo kuhusu mkasa wa Fukushima na tunahimiza kwamba viwanda vyote vinavyozalisha kawi ya nyuklia vifungwe sio tu kiwanda cha Takahama pekee yake,"alisema Kaido
Mwanaharakati anayepinga matumizi ya nguvu za nyuklia Tadashi Matsuda aliwashukuru waathirika wa mkasa huu kwa mchango wao katika kesi hiyo.
"Huu ni uamuzi uliofanyika, kutokana na msukumo wenu kama waathirika wa mkasa huu''.
Uamuzi huu ni pigo kubwa kwa serikali ya Japan ambayo inalenga kufufua sekta yake ya nyuklia.
Hadi sasa viwanda 48 vya kuzalisha nyuklia nchini humo vimefungwa kufuatia mkasa huo wa mwaka 2011.
Hata hivyo waziri mkuu wa Japan Yoshihide Suga, amesema serikali bado inamatumaini ya kufufua tena viwanda hivyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni