07 Aprili 2015

Mahari ni mzigo kwa wanaume?

Mwanamume mmoja kutoka upande wa kaskazini magharibi mwa Pakistan ,amempiga risasi mpenzi wake wa zamani na watu tisa wa familia ya mwanamke huyo mwishoni mwa wiki ;hata hivyo inaelezwa kuwa mwanamume huyo miezi sita iliyopita aliwaua wazazi wake pamoja na kaka zake wawili kwa kosa la kukataa kumlipia mahari.
Kijana huyo mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 25,ambaye polisi wamemtaja kwa jina la Mir Ahmad Shah,ambaye alikuwa mafichoni baada ya kufanya shambulizi la kutumia silaha kwa kutumia bunduki aina ya AK-47 katika wilaya ya Charsadda jimbo la Khyber Pakhtunkhwa.

Inaelezwa na mkuu wa polisi wa wilaya hiyo chief Shafiullah Khan, kuwa Ahmad aliivamia nyumba hiyo na kuwapiga risasi watu wa familia moja waliokuwa usingizini ,na kuongeza kusema kwamba watoto wawili na wanawake wane ni miongoni mwa waliouawa.
Khan amesema kwamba Shah alikuwa akisakwa kwa kesi ya mauaji ya nduguze ,mauaji aliyoyatekeleza mwaka wa jana ,familia ya Ahmad ilikataa kukubali mahari waliyotajiwa na wakwe zao ,baba wa mchumba wa kijana huyo ambaye sasa ni marehemu walitaka kiwanja cha makazi kama mahari ya binti huyo.
Polisi mwingine mwenye dhamana Gulzar Khan,amesema kwamba baada ya kijana huyo kuitekeketeza familia yake kwa mtutu wa bunduki, aliwageukia wakweze na kuwakosea adabu kwa mahari waliyoitaka kwao.
Polisi mpaka sasa wameamua kuimarisha ulinzi mipakani na katika maeneo ambayo kijana huyo angejaribu kutafuta hifadhi, na wameapa kumtia mkononi.
Ndoa nchini Pakistan hupangwa ,na mara nyingi maharusi huwa ni mabinamu.wazazi wa mwanamke wakati mwingine hudai mahari kubwa kama bima endapo ndoa yaweza kuvunjika kwa talaka.
Kulingana na jamii zingine,mahari katika dini ya kiislam hulipwa na mwanamume ama familia ya kijana kwa kumpa bi harusi wakati wa harakati za ndoa,na mahari hiyo yaweza kuwa zawadi ama pesa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728