15 Mei 2016

Kagame akana kuwasaidia waasi Burundi

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekana madai yaliotolewa na Umoja wa Mataifa kwamba taifa lake linaendelea kuwasaidia waasi katika nchi jirani ya Burundi.
Bw Kagame amesema kuwa tatizo la Burundi linatoka ndani ya nchi hiyo, na sio nje.
Burundi imekabiliwa na mgogoro mbaya wa kisiasa tangu rais Pierre Nkurunziza kuamua kupigania muhula mwengine mwaka uliopita.
Ni mwaka mmoja kamili tangu rais Nkurunziza kuepekua jaribio la mapinduzi.
Rwanda ilikana madai kama hayo kuhusu kuwaunga mkono waasi katika ripoti ya awali ya Umoja wa Mataifa mnamo mwezi Februari.
Bw Kagame amekosoa wachapishaji wa ripoti hiyo ambayo inatarajiwa kuwasilishwa katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa baadaye,ikisema mda wake ungetumika vyema kuangazia matatizo yanayokumba mataifa badala ya kuyazidisha.

Ripoti hiyo iliopatikana na chombo cha habari cha Reuters imeishtumu Rwanda kwa kutoa mafunzo pamoja na usaidizi wa kifedha kipindi chote cha mwaka 2016 kwa waasi wanaolenga kumuondoa madarakani rais Pierre Nkurunziza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728