21 Machi 2017

Mwanafunzi afariki baada ya kupigwa na Radi wakati akifua nguo

MWANAFUNZI wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Changwe wilayani humu, Chiza Daniel (14), mkazi wa Kijiji cha Changwe Wilaya ya Buhigwe mkoani
Kigoma, amefariki dunia papo hapo baada ya kupigwa na radi wakati akifua nguo nyumbani kwao.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Obadiah Nselu, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 7:00 mchana kijiji cha Changwe Kata ya Mubanga Tarafa ya Manyovu Wilaya ya Buhingwe.

Kamanda Nselu alisema mwanafunzi huyo alifariki dunia baada ya kupigwa na radi kiunoni akiwa anafua nguo zake nje ya nyumba yao.

Alisema mwili wa marehemu ulipelekwa Hospitali ya Mkoa Maweni na kufanyiwa uchunguzi kisha kukabidhiwa ndugu kwa maziko.

Aidha, Kamanda Nselu alisema mazishi ya marehemu yanatarajiwa kufanyika kesho katika Kijiji cha Changwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728