21 Machi 2017

Watangazaji Clouds Wavunja ukimya wavunja urafiki na Makonda

Toka sakata la Makonda kuvamia,nimejipa muda kuangalia hii Tv,vipindi na nyimbo wanazopiga ni kama wanafikisha ujumbe kwa mkulu na RC wa Dsm.Wanapiga nyimbo za "vijembe" na leo wameimba wimbo wa "Solidality Forever" huku wameshikana mikono studio.


Leo asubuhi nimeangalia kipindi cha "Clouds 360",nimesikiliza nukuu zilizotolewa na watangaji wote watatu, lakini nimefurahia zaidi nukuu ya pili ya mtangazaji Sam Sasali

"Kuanzia sasa nitasoma kila kitu, nitasoma kila gazeti liwe la michezo siasa na kila kitu sitaki kupangiwa, sitaki kupigiwa simu za maelekezo kwamba hiyo story soma au hiyo usisome"

Hii imetoa picha kuwa kumbe hawa jamaa huko nyuma walikuwa "wanatumika",walikuwa wanapangiwa nini cha kusoma na kujadili kwa maslahi ya watu fulani.

Ndio maana katika siku zote za sakata la "Bashite na vyeti feki",hawa Clouds inasemekana hawakulizungumzia sana wala kulijadili kwa mapana ktk vipindi vyao.Lakini toka jana na leo,kuanzia kipindi cha muziki cha XXL mpaka Alasiri ya Clouds Tv,mjadala wa vyeti ulianza kushika hatamu.

Huu ni ujumbe kwa hawa wamiliki wa vyombo vya habari,zama za unafiki zimekwisha,wasimamie ukweli,maana wengine wanashindwa kusimama na Clouds Media Group sbb kwa muda mrefu walikuwa kama tawi la chama na kitengo cha propaganda mpaka wengine "tukazila" kuwafuatilia.Hili ni fundisho kwao.

Source:JamiiForums/Barafu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728