17 Oktoba 2014

Mgogoro wa maiti Moshi waingia siku ya 43 leo

Moshi. Mgogoro wa kifamilia kuhusu mwenye haki ya kuzika mwili wa Rosemary Marandu (38), umeingia siku ya 43 leo, huku ukiendelea kuhifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mwili wa marehemu huyo aliyefariki dunia Septemba 4, mwaka huu umehifadhiwa hospitalini hapo na unalipiwa Sh9,000 kwa siku, gharama ambayo hadi leo imefika Sh387,000.
Akizungumza jana, baba wa marehemu, Flavian Marandu, alitoa ruksa ya kuzikwa mwili huo, huku akijiweka kando akidai hana mamlaka ya kuzika mke wa mtu.
Wiki moja iliyopita, mume wa marehemu, Sigfrid Mlingi alimtuhumu baba mkwe wake huyo kuzuia mwili huo na baadaye kumtolea lugha chafu.
“Mimi ndiye nilimuuguza Hospitali ya Mawenzi hadi kunifia mikononi, nilipokwenda Keryo na kuonana na baba mkwe, akanifukuza,” alidai Mlingi.
Mlingi alisema awali walikubaliana kumzika Septemba 9 katika Makaburi ya Karanga, Manispaa ya Moshi lakini baadaye mkwewe alikataa.
Lakini jana, Marandu alisema: “Huyo ni mke wa mtu...kama kuna mtu ana shida akachukue kibali akazike, mimi sina kibali,” alisema.
Marandu alisema tangu msiba huo utokee, ametuma marafiki zake kuzungumza na ndugu ili mazishi hayo yafanyike baada ya kuridhiwa na mume na mama mzazi lakini hawatoi ushirikiano.
Lakini ndugu mwingine wa marehemu, Bertha Akwilin alipoulizwa jana, alikiri kuzungumza na Marandu juzi na kumwelekeza kwenda kuchukua kibali kutoka kwa mtu aitwaye Tesha.
“Ni kweli nimepata bahati ya kuzungumza na baba (Marandu) na akatoa ruksa hiyo lakini mama wa marehemu na wana ndugu bado wanatafakari ukweli wa kauli ya Marandu,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728