21 Oktoba 2014

Tanzania inahitaji walimu laki nne ifikapo mwaka 2030

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO) hivi karibuni limetoa ripoti inayoonyesha Tanzania itahitaji angalau walimu 406,600, ifikapo mwaka 2030.
Wakati mahitaji ya walimu katika nchi mbalimbali yakizidi kuwa makubwa, shirika hilo linasema uhaba wa walimu wenye mafunzo unazidi kutamalaki katika nchi mbalimbali, ikiwamo Tanzania.
Kwa sasa na inawezekana na baadaye, Afrika ndiyo inayoongoza kwa kuwa na uhaba mkubwa wa walimu, jambo linalohatarisha mustakabali wa sekta ya elimu barani humu.
Ukiondoa Tanzania, ripoti hiyo inaonyesha mahitaji makubwa ya walimu pia yanazikabili nchi kadhaa za Afrika, zikiwamo Uganda, Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Kwa ngazi ya dunia ripoti hiyo inasema hadi mwaka huo, walimu zaidi ya milioni 27 watahitajika kuziba mapengo ya walimu wanaostaafu na nafasi mpya za ajira.
Hata hivyo, taarifa nzuri ya ripoti hiyo inaonyesha kama Tanzania itajipanga vizuri, inaweza kuziba pengo la walimu , hasa katika shule za msingi ifikapo mwaka 2026. Hilo linawezekana ikiwa nchi hiyo itakuwa inaajiri angalau asilimia 10 ya walimu kila mwaka.
Hata hivyo, Unesco inasema mikakati ya kuziba mianya hiyo ya walimu katika nchi nyingi imegubikwa na dosari kubwa kwa vyombo husika kuajiri walimu wasio na mafunzo bora ya ualimu.
“Takwimu zinaonyesha kuwapo kwa tatizo sugu la walimu wasio na mafunzo katika nchi nyingi. Kama hatua hazitochukuliwa, itakuwa vigumu kwa watoto wote kwenda shule na kujifunza,” inasema taarifa ya Unesco iliyotolewa kwa umma.
Sababu za uhaba wa walimu
Takwimu za Unesco zimetolewa wakati ambao kila mdau anapozungumzia maendeleo ya elimu, hakosi kutaja uhaba wa walimu kama moja ya changamoto tete zinazoikabili sekta hiyo nchini.
Walimu na wakuu wa shule wanalia na uhaba wa walimu, wadau wanalalamika, Serikali nayo inakiri kuwa walimu ni tatizo nchini.
Kwa nini Tanzania iwe na uhaba mkubwa wa walimu? Mwalimu mstaafu, 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728