09 Oktoba 2014

Madini ya Sh15.8 bilioni yakamatwa yakitoroshwa

Chalinze. Wakala wa Ukaguzi wa Madini nchini (TMAA), umekamata madini yenye thamani ya Sh15.8 bilioni yaliyokuwa yakitoroshwa kwenda nje ya nchi bila ya kibali na kukwepa kulipa kodi ya mapato.
Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Uzalishaji na Biashara ya Madini wa TMAA, Conrad Mtui alisema kuwa kiasi hicho cha madini aina mbalimbali kilikamatwa kati ya Julai, 2012 hadi Agosti, mwaka huu.
Mtui aliwaambia waandishi wa habari juzi katika ziara ya kutembelea migodi ya madini ya ujenzi ya Lugoba na Msolwa wilayani Bagamoyo, kuwa wakala ulikamata madini hayo katika matukio 53 ambayo yaliwahusisha mawakala wa madini.
“Baada ya kuanzisha madawati ya ukaguzi kwenye viwanja vya Kimataifa vya Ndege vya Julius Nyerere (JNIA), Kilimanjaro na Mwanza, tuliwakamata wote waliokuwa wakijaribu kusafirisha madini hayo kinyume cha sheria, matukio haya yanaweza pia kuongezeka muda wowote.





“Wahusika wamefikishwa mahakamani na baadhi yao wamehukumiwa na madini yao kutaifishwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010,” alisema Mtui.
Alipoulizwa kama kuna wachimbaji wakubwa waliokamatwa wakifanya hujuma hiyo, Mtui alisema waliokamatwa wengi walikuwa wafanyabiashara wadogo na madalali na hakukuwa na kampuni kubwa kwa kuwa kuna utaratibu maalumu wa ukaguzi na usafirishaji.
Hata hivyo, Mtui alisema baada ya kukaza uzi wa ukaguzi walifanikiwa kuongeza mrabaha kutoka kwenye migodi mikubwa ya dhahabu kiasi cha Dola za Marekani 427.98 kuanzia mwaka 2005 hadi mwishoni mwa Agosti mwaka huu.
“Wakala ulifanya ukaguzi na uhakiki wa madini yaliyozalishwa na kuuzwa na migodi mikubwa nchini. Ukaguzi huo ulisaidia kujua kiasi na thamani halisi ya madini yaliyozalishwa na kuuzwa kutoka migodi mbalimbali, ikiwamo saba ya dhahabu ya Geita, Golden Pride, Bulyanhulu, Tulawaka, North Mara, Buzwagi na New Luika,” alisema.
Pamoja na kujinadi kwa mafanikio hayo, Mtui alisema bado kuna ujanja wa utoroshaji kupitia njia za panya na upungufu wa rasilimali watu unawazuia kufanya ukaguzi katika migodi midogo, hivyo kuchangia upotevu wa mapato.
“Tuna wakaguzi wetu katika baadhi ya migodi midogo yenye uzalishaji mkubwa...lakini kwa mingine ni hasara kwa sababu unaweza kukuta malipo ya wakaguzi ni makubwa kuliko mrabaha unaopatikana,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728