21 Oktoba 2014

Diamond Platnumz: Bongofleva inakua kwa kasi kimataifa


Huenda akizungumza unaweza usimwelewe, lakini Diamond Platnumz aliamua kufikiri nje ya boksi na kufanikiwa kufanya kile alichokuwa akikikusudia, leo hii tayari makumi ya wasanii wameanza kutembea katika nyayo zake.



Kwa mujibu wa staa huyu ambaye alifanya mahojiano ya ana kwa ana nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam, anasema lilikuwa ni wazo lake tangu mwaka 2009 alipoingia rasmi katika muziki kwa kuweka nadhiri kwamba lazima ahakikishe anaitangaza nchi yake kupitia sanaa.
Anasema ilikuwa safari ndefu yenye milima na mabonde, lakini amefanikiwa kufikia hatua za mwanzo na anaamini bidii ikiongezwa kwake na wasanii wengine, muziki huo utafika mbali.
“Muziki wa Tanzania kwa sasa unaenda kasi mno, ukiangalia msanii Shetta wimbo wake wa ‘Kerewa’ unapigwa karibu redio za Fm sita hivi tunavyoongea wiki hii, wimbo wake umeshika nafasi ya tatu kwenye Beat Fm ya jijini Lagos, zamani kibongobongo suala kama hili lilikuwa ndoto na halikuwezekana kabisa.”
Diamond anasema mitandao ya kijamii imechangia kukua kwa soko lao, lakini jitihada binafsi za wao wenyewe zimesaidia.
“Ukiangalia katika vyombo vya habari hasa mitandao namna watu wanavyojitangaza, video zinavyofanyika ni tofauti na zamani. Tulikuwa tunafanya muziki lakini tulikuwa hatujitangazi, sasa hivi msanii akitoa singo anatengeneza kava, matangazo, watu wanafanya muziki kama biashara, wanapanda jukwaani na madansa yaani nidhamu ipo katika muziki tofauti na zamani,”.
Hata hivyo, Diamond anasema anakumbana na changamoto nyingi hivi sasa katika maandalizi ya kazi zake kwani ana soko kubwa la ndani lakini pia soko pana la nje ambako analazimika kuwalisha mashabiki wake wapya.
“Mwenyezi Mungu kanijalia kuna mashabiki wananikubali na wananiamini ndani na nje ya nchi, changamoto ninayoipata kwa sasa ni kuhusu mashairi ya kazi zangu, nitatengeneza vipi wimbo ambao nje utaeleweka?” anahoji na kuongeza:
“Soko la Tanzania linachanganya, watu wanataka niimbe mtu kaachwa lakini mwenyewe naangalia hivi wimbo kama huu nje utakubalika? Yaani hicho ndiyo kitu kinachokuwa kinanivuruga akili yangu kwa hiyo inabidi huku nifanye wimbo wake na nje wake ndiyo maana hata ukiangalia katika wimbo wa ‘Bum Bum’ na ‘Mdogo Mdogo’ kuna vionjo tofauti,” anasema.
Licha ya ugumu wa kazi aliyonayo, anasema bado mapromota wamekuwa wagumu kuelewa na kurekebisha malipo ya wasanii, tatizo linalosababisha wengi kukata tamaa.
“Ningependa tukimbizane katika soko la kimataifa, lakini tatizo wasanii walio wengi na wenye uwezo wanalipwa malipo kiduchu yasiyolingana na kazi zao, wataweza vipi kufanya kazi zenye viwango kama ninavyofanya mimi?”
“Tatizo lipo kwa hawa mapromota, mtu hataki kukubali kwamba kuna kitu kimebadilika, kukubali kwamba wasanii nao wapo katika soko na inatakiwa muziki ubadilike, mapromota wakubali kwamba tunataka haya yarekebishwe ili muziki ubadilike malipo ya shoo yapande wasanii bado wananyonywa, lakini mimi sikubali hata siku moja ndiyo maana nimejitengenezea jina langu kwenye biashara,” anasema Diamond.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728