24 Oktoba 2014

Madaktari Australia wapandikiza moyo



Madaktari wa Australia wamefanikiwa kuwarejeshea uhai wagonjwa watatu baada ya kupandikizwa moyo uliokufa katika operesheni ya kwanza kufanyika duniani.
Madaktari katika hospitali ya St Vincent mjini Sydney walitumia dawa ya kuzuia kuharibika iliyotengenezwa na Taasisi ya Utafiti wa Moyo ya Victor Chang kwa kupandikiza viungo kwa Michelle Gribilas,mwenye umri wa miaka 57 na Jan Damen mwenye umri wa miaka 44, huku mgonjwa wa tatu akiendelea kupona.

Moyo mmoja, ulisimama mapigo kwa dakika 20 kabla ya kuurejesha katika uhai, ukiwa umewekwa katika mashine na kuuchoma dawa ya kuzuia kuharibika.
Jan Damen na mkewe Silvana

Jan Damen, mwenye umri wa miaka 44, (akiwa katika picha na mke wake Silvana) alipandikizwa moyo uliokufa na kuupa uhai.

Wagonjwa wawili waliopandikizwa moyo (Michelle Gribilas, kushoto, na Bwana Damen, katikati) wanazungumza na daktari wa upasuaji Kumud Dhital

Moyo unahuishwa baada ya kupoteza uhai na kupandikizwa. Hospitali hiyo inaamini asilimia 30 za watu watarejeshewa uhai kutokana na kugunduliwa kwa dawa hii, ambayo hupunguza kiwango cha uharibifu kwenye moyo na kuwa tayari kupandikizwa.
Michelle Gribilas (kushoto) Jan Damen(katikati) wakizungumza na daktari wao Kumud Dhital
Kabla ya operesheni hizi, madaktari wa moyo wamekuwa wakitumia moyo kutoka kwa watu waliokufa kwa asilimia 100 ambao katika uhai wao walitaka viungo vyao vitumiwe na watu wengine wenye kuhitaji, lakini sasa upatikanaji wa moyo utaongezeka zaidi.

Dawa hiyo iliyochukua miaka 12 kuitengeneza, pia inasaidia kuimarisha kazi ya moyo ambao unatolewa baada ya kifo (DCD) wakati ukianzishwa kufanya kazi upya.

Bi Gribilas, ambaye amestaafu na kuishi Campsie kusini magharibi mwa Sydney, amesema ni mtu tofauti kwa sasa baada ya kupandikizwa moyo mpya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728