22 Septemba 2016

Rais Buhari aiomba UN ijadiliane na Boko Haram

Hatima ya wasichana hao wa Chibok haijulikaniRais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amekaribisha Umoja wa mataifa kujadiliana na Boko Haram katika kutafuta kumaliza uasi wa miaka 7 wa wanamgambo hao wa kiisalmu na kuwaokoa zaidi ya wasichana 200 wa shule waliotekwa kutoka Chibok.
Amesema yupo tayari kuwaachia wanamgambo waliokamatwa wa Boko haram ili kupata uhuru wa wasichana waliotekwa.
Lakini amesema ni vigumu
kutambua nani kiongozi katika kundi hilo baada ya kuzuka mgawanyiko katika uongozi mwaka huu.

Buhari alikuwa akizunguma pembezoni mwa mkutano wa baraza kuu la Umoja wa mataifa New York.
Kutekwa kwa wasichana hao wa shule kulisababisha kuzuka kwa kampeni ya #BringBackOurGirls, ilioungwa mkono na mkewe rais wa Marekani Michelle Obama na mwanaharakati wa Pakistani Malala Yousafzai.
Mpaka sasa ni msichana mmoja pekee wa shule aliopatikana baada ya kuzuiwa kwa miaka miwili.
Katika mizei minane iliyopita, Boko Haram imepokonywa udhibiti wa sehemu nyingi baada ya kusukumwa nyuma katika operesheni ya jeshi la nchi na mataifa jirani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728