31 Desemba 2014

Kwa heri mwaka 2014 ulionogeshwa na filamu ya Katiba na Escrow

Hatmaye miezi 12 imekamilika leo ikiashiria kumalizika kwa mwaka 2014 utakaokumbukwa na wengi kwa kuwa na matukio motomoto.

TMA yatahadharisha wananchi kuhusu ongezeko la joto

Dar es Salaam. Mvua kubwa isiyotabirika inatarajiwa kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini hasa katika ukanda wa Pwani ya Kaskazini, maeneo ya Dar es Salaam, Tanga, Unguja na Pemba; pia katika ukanda wa Kaskazini Mashariki kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

Dereva wa bodaboda auwawa kinyama

Tanga. Watu wasiojulikana wamevamia nyumba ya dereva wa bodaboda, Omari Shaaban (32) na kumuua kisha kuichoma moto, katika tukio linalohusishwa na visa na wivu wa mapenzi.

Siku za wauza unga zahesabika china

Dar es Salaam. Siku za wasafirishaji na wauzaji wa dawa za kulevya kwenda China sasa zinahesabika baada ya Jeshi la Polisi na kitengo chake cha Dawa za Kulevya kubaini majina ya vigogo wanaofanya shughuli hiyo na kusema imeanza kuwashughulikia kimyakimya.

30 Desemba 2014

Dk. Slaa, polisi wapambana Dar

slaaHALI ya tafrani ilizuka jijini Dar es Salaam jana, baina ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa na askari wa Jeshi la Polisi.

Pengo aonya ufujaji wa Escrow

pgIKIWA imebaki miezi 10 kufikia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amewataka Watanzania walio masikini kuungana ili kuwang’oa madarakani viongozi matajiri wasiojali maslahi ya taifa.

Nyalandu atangaza kugombea urais

Pg 3.MBIO za urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimechukua sura mpya baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, kutangaza rasmi nia ya kugombea urais mwaka 2015.

25 Desemba 2014

Kambi ya jeshi la AU yavamiwa Somalia

Wapiganaji wa Al shabaab wamefanya shambulizi katika kambi kuu ya jeshi la Umoija wa Afrika karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu Somali.

Indonesia wakumbuka Tsunami

Wananchi wa Indonesia wameanza kuadhimisha mwaka wa kumi tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi lililosababisha mawimbi makubwa katika bahari ya Hindi, tsunami na kusababisha vifo vya watu zaidi ya watu laki mbili na elfu ishirini katika eneo kubwa.

Mtu aliyetabiri mwisho wa dunia afariki

Kiongozi mmoja wa dini ambaye alipata umaarufu nchini Kenya kwa kutabiri mwisho wa dunia mwaka 2006 amezikwa katika kijiji cha Bomet.

Filamu yenye utata yawekwa mitandaoni

Kampuni ya Sony Pictures imesema kuwa sinema yenye utata ya ucheshi kuhusu namna ya kumuuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, imewekwa katika mitandao Nchini Marekani.

24 Desemba 2014

Ajali

Ajali ya gari yachukua maisha ya wawili papo hapo muda mfupi uliopita huko Nzega. Chanzo chadaiwa ni mwendo kasi na mvua.

usajili wa Messi mtihani kwa Chelsea

Kocha wa Timu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kwa sasa hawana nafasi ya kumsaini mchezaji Lionel Messi kwa kuwa hakuna Fedha ya kutosha kumsajili mchezaji huyo .

Matic asema Chelsea itashinda mataji 4

Mchezaji wa kilabu ya Chelsea Nemanja Matic amesema kuwa anaamini kuwa kilabu hiyo itashinda mataji manne msimu huu.

Waziri mkuu mpya aidhinishwa Somali

Bunge la Somalia limeidhinisha uteuzi wa waziri mkuu mpya akiwa ni afisa wa tatu kuhudumu katika wadhfa huo katika kipindi cha miaka miwili.

Frank Lampard kusalia Manchester City

Bosi wa Manchester City Manuel Pellegrini anaamini watambakisha kiungo Frank Lampard.

IS:Yadungua ndege ya jeshi la muungano

Wapiganaji wa Islamic State nchini Syria wamedai kuidungua ndege ya kivita ya muungano wa jeshi unaoongozwa na Marekani.

Sakata la Escrow bado

Nchini Tanzania mtikisiko wa matokeo ya kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow umeendelea baada ya Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake. Maswi anakuwa kiongozi wa tatu wa ngazi ya juu kukumbwa na upepo huo akitanguliwa na Mwanasheria mkuu wa serikali ambaye alijiuzulu mwenyewe na Waziri wa Ardhi aliyetimuliwa kazi hadharani na Rais Jakaya Kikwete. Licha ya kuondoka kwa viongozi hao bado baadhi ya wananchi na vyama vya upinzani wameendelea kulalamika kuwa juhudi za kutekeleza maazimio ya Bunge ni ndogo. Kuhusiana na hilo Baruan Muhuza wa BBC alizungumza na Neville Meena, katibu wa Jukwaa la wahariri Tanzania.

Suarez atoa zawadi ya krismasi

mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez ametoa zawadi kwa watoto 500 na familia zao.

Vilabu vya Ulaya na Tetesi za usajili .

Uongozi wa Timu ya Manchester United umesema upo tayari kutoa paundi milioni 120 kwaajili ya kumsajili winga Gareth Balle mwenye umri wa miaka 25 kwa mwezi januari kutoka klabu ya Real Madrid , winga ambaye ni miongoni mwa wachezaji ghali zaidi ulimwenguni.
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728