24 Septemba 2014

Ebola:Wahudumu wengine washambuliwa


Shirikisho la kimataifa la msalaba mwekundu, limesema kuwa kikundi kingine cha wahudumu wa afya kilishambuliwa Jumanne Kusini Mashariki mwa Guinea walipokuwa wanakusanya miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola.
Mfanyakazi mmoja wa shirika hilo, anauguza majeraha baada ya kujeruhiwa vibaya katika shambulizi hilo katika eneo la Forecariah.
Kulingana na mkazi mmoja, jamaa wa wagonjwa waliofariiki walianza kuwashambulia wafanyakazi hao sita wa kujitolea , na kuharibu magari yao pamoja na kuwashambulia kwa mawe wafanyakazi hao.
Huu ni uvamizi wa hivi karibuni dhidi ya wahudumu wa afya ambao bila shaka unatatiza juhudi za kupambana na ugonjwa huo mkali.
Wiki jana madaktari wengine na wandishi wa habari walishambuliwa Magharibi mwa nchi hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728