29 Septemba 2014

Dereva bodaboda atuhumiwa kumtorosha mwanafunzi

DEREVA wa pikipiki (bodaboda) Emanuel Kahemela aliyehukumiwa kifungo cha uangalizi kwa mwaka mmoja nje katika kesi ya kubaka kwa kuishi na binti (jina linahifadhiwa) mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Mlamke ya Halmashuri ya Manispaa Iringa, amemtorosha tena.

Kahemela, alimtorosha binti huyo kwa kipindi cha miezi mitatu na kwenda kuishi naye kinyumba kabla ya kukamatwa na kuhukumiwa kifunguo hicho ambacho alikiuka.

Akizungumza na Tanzania Daima, Yusuph Mwimbage, alisema Kahemela alifunguliwa kesi ya kubaka na polisi yenye namba IR/RB/5156/2014, ambayo ilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Iringa, ambako Hakimu John Mpitanjia alitoa hukumu hiyo.

Mwimbage, alisema baada ya hukumu hiyo Kihemela alirudi nyumbani kwa mlezi wa binti huyo Amina Mwimbage, ambako alifanya vurugu kisha kumtorosha tena binti huyo.

Alisema walipofuatilia mahakamani walibaini hukumu ilitolewa bila walezi wa binti huyo kuwepo hali inayozua shaka, kwa kuwa walipofuatilia walibaini kulikuwa na ujanja umefanyika kupunguza umri wa Kahemela, kutoka miaka 21 hadi 17.

Alisema ujanja huo ulifanywa kwa lengo la kumuepusha kijana huyo kuhukumiwa kama mtu mzima, kwa kuwa sheria inatambua umri wa mtu mzima unaanzia miaka 18.

“Sisi tunaomba ngazi za juu zilifuatilie suala hili maana tunaona haki inaminywa, binti yetu ameachishwa shule na kutoroshwa….hii si haki hata kidogo,” alisema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728