31 Oktoba 2014

Lowassa, Makamba ‘wagongana’ kanisani

Mahenge. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba wamewaomba viongozi wa dini kuwasamehe viongozi wa Serikali waliokwaruzana nao wakati wa mchakato wa Katiba na kuliombea Taifa lipate viongozi wenye hekima na uwezo katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Usipitwe kamwe

Changia upate mibaraka na Bwana atukuzwe

26 Oktoba 2014

TEMBEA UYAONE

Duniani kuna mambo jamani angalia hapa

Chelsea yaapa kuichapa Man United

Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa viongozi hao wa ligi ya Uingereza watajaribu kuimarisha mchezo wao dhidi ya Manchester United siku ya jumapili.

Jionee maajabu mzee azikwa akiwa ameketi

Je,katika utamaduni wenu kiongozi wa kijiji,mganga wa kienyeji na mkulima mashuhuri huzikwa vipi?.

25 Oktoba 2014

Mourinho amwaga sifa za kutosha kwa Van gaal



Mkufunzi wa timu ya Manchester Louis van Gaal amesisitiza kuwa hakuchukuwa jukumu kubwa la kumfanya Jose Mourinho kuwa miongoni mwa wakufunzi waliofaulu duniani.


Madrid yafanya kufuru

Hatimaye madrid yafanya kufuru ya kuangusha kipigo cha mabao matatu kwa moja kwa maasimu wao bacelona baada ya kuja na bonge la come back,cristiano akisawazisha na huku pepe akiongeza la pili na baada ya hapo hatimaye benzema akiufunga ukurasa wa mabao na mwisho ubao wa matokeo yakisomeka madrid 3 baca 1




HITIMISHO LA MKUTANO MKUBWA WA INJILI ULIOFANYIKA MANZESE WATU ZAIDI YA SABINI WAMEBATIZWA

Ni katika shamra shamra na hekaheka za hitimusho la mkutano wa injili ulioandaliwa na kanisa la waadventista wasabato manzese ulio udhuriwa na watu mamia ya watu kusikiliza na kufahamu kweli Mungu. Wachungaji mbalimbali wakihudumu katika mkutano huo. na kwaya mbali mbali zikiwa zimealikwa kuhudumu katika mkutano huo






Kura ya Maoni mkorogano


Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Ruaha, Profesa Gaudence Mpangala alisema, “Tangu mwanzo niliupinga mchakato wa Katiba na matokeo yake imezaliwa Katiba Inayopendekezwa isiyokuwa na maoni muhimu ya Watanzania. Sikubaliani na mchakato wa kura ya maoni.”Profesa Mpangala alisema mchakato wa kupata Katiba Mpya unatakiwa kurudiwa mwaka 2016 kwa maelezo kuwa Katiba itakayopatikana haitakuwa na ridhaa kwa Watanzania.

24 Oktoba 2014

SOKONI: Balotelli kupigwa mnada Januari

Pinda atangaza rasmi kuwania urais


Diamond akabidhi ‘kombati’

Dar es Salaam. Mwanamuziki Nassib Abdul, ‘Diamond Platnumz’ amesalimisha nguo zake za kijeshi kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Madaktari Australia wapandikiza moyo



Madaktari wa Australia wamefanikiwa kuwarejeshea uhai wagonjwa watatu baada ya kupandikizwa moyo uliokufa katika operesheni ya kwanza kufanyika duniani.
Madaktari katika hospitali ya St Vincent mjini Sydney walitumia dawa ya kuzuia kuharibika iliyotengenezwa na Taasisi ya Utafiti wa Moyo ya Victor Chang kwa kupandikiza viungo kwa Michelle Gribilas,mwenye umri wa miaka 57 na Jan Damen mwenye umri wa miaka 44, huku mgonjwa wa tatu akiendelea kupona.

Moyo mmoja, ulisimama mapigo kwa dakika 20 kabla ya kuurejesha katika uhai, ukiwa umewekwa katika mashine na kuuchoma dawa ya kuzuia kuharibika.
Jan Damen na mkewe Silvana

Jan Damen, mwenye umri wa miaka 44, (akiwa katika picha na mke wake Silvana) alipandikizwa moyo uliokufa na kuupa uhai.

Wagonjwa wawili waliopandikizwa moyo (Michelle Gribilas, kushoto, na Bwana Damen, katikati) wanazungumza na daktari wa upasuaji Kumud Dhital

Moyo unahuishwa baada ya kupoteza uhai na kupandikizwa. Hospitali hiyo inaamini asilimia 30 za watu watarejeshewa uhai kutokana na kugunduliwa kwa dawa hii, ambayo hupunguza kiwango cha uharibifu kwenye moyo na kuwa tayari kupandikizwa.
Michelle Gribilas (kushoto) Jan Damen(katikati) wakizungumza na daktari wao Kumud Dhital
Kabla ya operesheni hizi, madaktari wa moyo wamekuwa wakitumia moyo kutoka kwa watu waliokufa kwa asilimia 100 ambao katika uhai wao walitaka viungo vyao vitumiwe na watu wengine wenye kuhitaji, lakini sasa upatikanaji wa moyo utaongezeka zaidi.

Dawa hiyo iliyochukua miaka 12 kuitengeneza, pia inasaidia kuimarisha kazi ya moyo ambao unatolewa baada ya kifo (DCD) wakati ukianzishwa kufanya kazi upya.

Bi Gribilas, ambaye amestaafu na kuishi Campsie kusini magharibi mwa Sydney, amesema ni mtu tofauti kwa sasa baada ya kupandikizwa moyo mpya.

22 Oktoba 2014

Football scores

Uefa  hapatoshi huku majogoo wa jiji wakikaa tatu mtungi kutoka kwa madrid

21 Oktoba 2014

Diamond Platnumz: Bongofleva inakua kwa kasi kimataifa


Huenda akizungumza unaweza usimwelewe, lakini Diamond Platnumz aliamua kufikiri nje ya boksi na kufanikiwa kufanya kile alichokuwa akikikusudia, leo hii tayari makumi ya wasanii wameanza kutembea katika nyayo zake.

Sugu: Samuel Sitta alisaliti ahadi yake

Mwanasiasa huyo kijana pia amemtetea aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman kwa kukataa vipengele 22 kwenye Katiba Inayopendekezwa, akisema alitoa maoni yake binafsi kama alivyofanya Rais Jakaya Kikwete wakati akizindua Bunge la Katiba mwezi Machi.

Dar es Salaam. Ikiwa ni takriban majuma mawili sasa tangu Bunge la Maalumu la Katiba likamilishe kazi ya kuandika Katiba Inayopendekezwa, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesema anajuta kumchagua Samuel Sitta kuwa mwenyekiti wa chombo hicho, akidai kuwa amesaliti ahadi yake kwa wapinzani wakati akiomba kura.
Katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Mbilinyi alimtuhumu Sitta kuwa aliwageuka wapinzani baada ya kuchaguliwa kuongoza chombo hicho cha kihistoria kwa kuweka mbele masilahi yake binafsi na Chama cha Mapinduzi (CCM) badala ya wananchi wote, kama alivyoahidi wakati akiomba kura za kuwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba.
Sitta, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Bunge la Tisa, alionekana anakubalika na pande zote, CCM na wapinzani, na hivyo chama hicho kumpitisha kuwania uenyekiti wa Bunge la Katiba ambao alishinda kwa kupata asilimia 86.5 dhidi ya mpinzani wake, Hashim Rungwe Sipunda aliyepata asilimia 12.3. “Najuta kumfanyia Sitta kampeni,” alisema Mbilinyi, msanii wa muziki wa rap ambaye mashairi ya baadhi ya nyimbo zilizompatia umaarufu yalikuwa yamejaa utetezi wa haki.
“Wakati wa kampeni, Sitta alinifuata kwa upole akiniomba nimpigie debe ili akishinda, atekeleze pamoja na mambo mengine, madai ya serikali tatu yaliyotolewa na wajumbe wa upinzani,” alisema Mbilinyi ambaye jina lake maarufu la kisanii ni Sugu.
“Sitta alikuja kwangu na kuniambia ‘Sugu unajua kuwa una kura zangu 100 za wajumbe kutokana na ushawishi wako kwa vijana na hata wajumbe wa CCM?’
“Mimi nilimuuliza ‘kwa nini nikupe kura 100?’ Sitta huyu huyu akanijibu ‘unajua mkimchagua (Andrew) Chenge ana msimamo wa serikali mbili, lakini wananchi wanataka serikali tatu. Mkinichagua mimi nitasimamia hilo,” alidai Sugu.
Hata hivyo, Chenge hakuingia kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya vikao vya ndani vya CCM kumpitisha Sitta. Badala yake, Chenge aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi.
Julai mwaka jana, Sitta alikaririwa akiunga mkono serikali tatu, lakini akapinga nchi kuongozwa na marais watatu akisema wakuu wa Zanzibar na Bara wawe na hadhi nyingine badala ya urais, huku akipendekeza kuwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania libadilishwe na kuwa Shirikisho la Nchi za Tanzania.
Hata hivyo, Mbilinyi anaona huo ulikuwa ujanja. “Sitta alitumia ujanja ujanja kufika pale ili afanye ya kwake binafsi kufikisha maoni yake na ninashukuru kuwa amejidhihirishia kuwa ameanguka katika harakati za urais mwakani na hatakuwapo katika mchakato huo,” alisema Mbilinyi.
“Ninajuta kumpa kura yangu na ninajuta kwa wajumbe wa 201 kumpa kura Sitta kwani ameshindwa kusimamia kile alichokiahidi.”
Sitta, mbunge wa Urambo Mashariki na ambaye anatajwa kuwania urais mwakani kwa tiketi ya CCM, alianza kusakamwa kutokana na kumruhusu Rais Jakaya Kikwete kuzindua Bunge la Katiba baada ya mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kusoma hotuba yake na kuwasilisha Rasimu ya Katiba, kitendo kilichomruhusu mkuu huyo wa nchi kuchambua baadhi ya vipengele na kutoa maoni yake.

Ligi ya mabingwa ulaya kimenuka


Tanzania inahitaji walimu laki nne ifikapo mwaka 2030

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO) hivi karibuni limetoa ripoti inayoonyesha Tanzania itahitaji angalau walimu 406,600, ifikapo mwaka 2030.
Wakati mahitaji ya walimu katika nchi mbalimbali yakizidi kuwa makubwa, shirika hilo linasema uhaba wa walimu wenye mafunzo unazidi kutamalaki katika nchi mbalimbali, ikiwamo Tanzania.
Kwa sasa na inawezekana na baadaye, Afrika ndiyo inayoongoza kwa kuwa na uhaba mkubwa wa walimu, jambo linalohatarisha mustakabali wa sekta ya elimu barani humu.
Ukiondoa Tanzania, ripoti hiyo inaonyesha mahitaji makubwa ya walimu pia yanazikabili nchi kadhaa za Afrika, zikiwamo Uganda, Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Kwa ngazi ya dunia ripoti hiyo inasema hadi mwaka huo, walimu zaidi ya milioni 27 watahitajika kuziba mapengo ya walimu wanaostaafu na nafasi mpya za ajira.
Hata hivyo, taarifa nzuri ya ripoti hiyo inaonyesha kama Tanzania itajipanga vizuri, inaweza kuziba pengo la walimu , hasa katika shule za msingi ifikapo mwaka 2026. Hilo linawezekana ikiwa nchi hiyo itakuwa inaajiri angalau asilimia 10 ya walimu kila mwaka.
Hata hivyo, Unesco inasema mikakati ya kuziba mianya hiyo ya walimu katika nchi nyingi imegubikwa na dosari kubwa kwa vyombo husika kuajiri walimu wasio na mafunzo bora ya ualimu.
“Takwimu zinaonyesha kuwapo kwa tatizo sugu la walimu wasio na mafunzo katika nchi nyingi. Kama hatua hazitochukuliwa, itakuwa vigumu kwa watoto wote kwenda shule na kujifunza,” inasema taarifa ya Unesco iliyotolewa kwa umma.
Sababu za uhaba wa walimu
Takwimu za Unesco zimetolewa wakati ambao kila mdau anapozungumzia maendeleo ya elimu, hakosi kutaja uhaba wa walimu kama moja ya changamoto tete zinazoikabili sekta hiyo nchini.
Walimu na wakuu wa shule wanalia na uhaba wa walimu, wadau wanalalamika, Serikali nayo inakiri kuwa walimu ni tatizo nchini.
Kwa nini Tanzania iwe na uhaba mkubwa wa walimu? Mwalimu mstaafu, 

17 Oktoba 2014

Vijana someni Katiba Inayopendekezwa

Njombe. Vijana wametakiwa kuisoma Katiba Inayopendekezwa kwa umakini na kuvielewa vipengele vilivyopo katika Ibara zote ili wafanye uamuzi sahihi.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Njombe, Luca Mgaya alitoa rai hiyo mjini hapa jana.
Alisema vijana wakiielewa Katiba wataepuka vishawishi vya nini wafanye kutoka katika makundi mbalimbali, yakiwamo ya kisiasa.
Alisema vijana wana wajibu wa kuhakikisha wanafuatilia vyema Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa kwa kupata nakala yake na kuisoma ili kuelewa mambo yaliyomo.
Alisema vijana wanapaswa kujiepusha kushikiwa akili na makundi yanayopita kuwashawishi kuikubali rasimu hiyo au kuikataa, badala yake waisome na kutoa uamuzi wao.
“Kuna makundi yanasema kuna vipengele vya msingi vimeondolewa katika Rasimu ya Tume ya Jaji Joseph Warioba, wengine wanasema Rasimu ni nzuri, iungeni mkono.
“Sisi vijana kabla ya kufanya uamuzi wowote, lazima tuipate nakala ya Rasimu hiyo tuisome kipengele kwa kipengele ili tuelewe kilichomo ndipo tufanye uamuzi,” alisema.
Alisema kama watabaini kuna vipengele vya msingi vimeondolewa katika Rasimu hiyo, watahoji vimeondolewa kwa sababu gani ili kupata ufafanuzi.
Pia aliwataka vijana kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Desemba mwaka huu na Uchaguzi Mkuu mwakani.
Aliwataka vijana kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura pindi litakapoanza kuboreshwa ili waweze kutumia vyema haki yao ya kuchagua na kuchaguliwa.

Mgogoro wa maiti Moshi waingia siku ya 43 leo

Moshi. Mgogoro wa kifamilia kuhusu mwenye haki ya kuzika mwili wa Rosemary Marandu (38), umeingia siku ya 43 leo, huku ukiendelea kuhifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mwili wa marehemu huyo aliyefariki dunia Septemba 4, mwaka huu umehifadhiwa hospitalini hapo na unalipiwa Sh9,000 kwa siku, gharama ambayo hadi leo imefika Sh387,000.
Akizungumza jana, baba wa marehemu, Flavian Marandu, alitoa ruksa ya kuzikwa mwili huo, huku akijiweka kando akidai hana mamlaka ya kuzika mke wa mtu.
Wiki moja iliyopita, mume wa marehemu, Sigfrid Mlingi alimtuhumu baba mkwe wake huyo kuzuia mwili huo na baadaye kumtolea lugha chafu.
“Mimi ndiye nilimuuguza Hospitali ya Mawenzi hadi kunifia mikononi, nilipokwenda Keryo na kuonana na baba mkwe, akanifukuza,” alidai Mlingi.
Mlingi alisema awali walikubaliana kumzika Septemba 9 katika Makaburi ya Karanga, Manispaa ya Moshi lakini baadaye mkwewe alikataa.
Lakini jana, Marandu alisema: “Huyo ni mke wa mtu...kama kuna mtu ana shida akachukue kibali akazike, mimi sina kibali,” alisema.
Marandu alisema tangu msiba huo utokee, ametuma marafiki zake kuzungumza na ndugu ili mazishi hayo yafanyike baada ya kuridhiwa na mume na mama mzazi lakini hawatoi ushirikiano.
Lakini ndugu mwingine wa marehemu, Bertha Akwilin alipoulizwa jana, alikiri kuzungumza na Marandu juzi na kumwelekeza kwenda kuchukua kibali kutoka kwa mtu aitwaye Tesha.
“Ni kweli nimepata bahati ya kuzungumza na baba (Marandu) na akatoa ruksa hiyo lakini mama wa marehemu na wana ndugu bado wanatafakari ukweli wa kauli ya Marandu,” alisema.

Warioba: Msikurupuke kupitisha Katiba Mpya

Bunda. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewataka Watanzania kutokurupuka kuipitisha Katiba Inayopendekezwa kwa kuwa imeyaacha kando maoni yao mengi na akawataka waisome kwa makini kabla ya kuikubali au kuikataa.
Akiwa katika likizo ya wiki moja nyumbani kwake Bunda, Mkoa wa Mara, Jaji Warioba alialikwa na vijana wa mji huo kupitia Jukwaa lao la Uwazi na Fikra Yakinifu, wakiomba azungumze nao kuhusu masuala mbalimbali hasa mchakato wa Katiba Mpya.
Katika mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Harrieth, Jaji Warioba aliulizwa na kujibu maswali; anaionaje Katiba Inayopendekezwa na iwapo CCM imemgeuka kwa nini asihame chama?
Akijibu maswali hayo, Jaji Warioba alisema Katiba hiyo haina maoni yote ya wananchi kama Bunge Maalumu lilivyojinadi, bali yamewekwa machache ambayo hata hivyo yamo hata katika Katiba ya sasa.
Kwa kufanya hivyo, alisema wajumbe hao walionyesha wanafurahishwa na hali iliyopo ya viongozi kukosa uzalendo, uadilifu na kukosa uwajibikaji hata kuwasababishia Watanzania maisha magumu ambayo kupitia maoni yao, walikuwa wameyatafutia dawa kwa kupendekeza maadili yatambulike kikatiba.
Mathalan, alisema wananchi wengi walipendekeza kiwepo kipengele cha maadili ya viongozi ili kuwadhibiti dhidi ya vitendo viovu wanavyovifanya kwa sasa kama ufisadi, rushwa na matumizi mabaya ya madaraka, lakini wajumbe wa Bunge walikirekebishana hadi kikapoteza maana.
Alisema wananchi walipendekeza muundo wa muungano wa serikali tatu ili kuondoa matatizo yaliyopo, kupatiwa madaraka ya kuwawajibisha wabunge wao pamoja na rais kupunguziwa madaraka, mambo ambayo yameondolewa na Bunge hilo Maalumu.
“Kazi yetu kama Tume ya kuandaa Katiba ya Watanzania tuliimaliza. Bunge nalo limemaliza kazi yake japo ina upungufu. Sasa kazi imebaki kwenu wenye Katiba; kuisoma iliyopendekezwa kwa makini kabla ya kuipigia kura,” alisema Warioba.
Jaji Warioba alieleza kusikitishwa na taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge la Katiba, Samuel Sitta siku ya kukabidhi Katiba Inayopendekezwa kwa Rais, kwamba Bunge hilo limeweka ndani ya katiba hiyo asilimia 81 ya maoni ya Tume, akisema huo ni uongo mkubwa.
“Ukweli ni kwamba wamechukua asilimia 20 tu na kutupa nje asilimia iliyobaki na kubandika yaliyomo katika Katiba ya sasa ambayo hayawezi kuleta mabadiliko yoyote,” alisema Jaji Warioba.
Hivyo, Jaji Warioba aliwataka Watanzania kwa umoja wao bila kujali tofauti zao za kisiasa, dini, rangi, kabila kuhakikisha kuwa wanapata Katiba Inayopendekezwa na kutumia muda mwingi kuisoma kabla ya kuipigia kura na kuwa wakikurupuka watajuta siku za usoni.
Akizungumzia hatima ya Muungano wa serikali mbili uliopo kwa sasa, Warioba alisema hachelei kusema kwamba huenda ukakumbana na changamoto nyingi siku za usoni iwapo wananchi watauridhia kupitia kura yao kwa vile asilimia kubwa ya Wazanzibari hawaukubali.

Majeruhi wa moto wazidi kupoteza maisha Dar

Dar es Salaam. Majeruhi wa moto uliotokana na mlipuko wa lori la mafuta huko Mbagala Rangi Tatu, Dar es Salaam wameendelea kupoteza maisha baada ya wengine wawili kufariki dunia na kufanya idadi yao kufikia saba.
Lori mali ya Kampuni ya Moil Transporter lililokuwa likisafirisha mafuta ya petroli kwenda Kampala, Uganda lilipinduka likiwa na lita 38,000 na kisha kuwaka moto.
“Hata hivyo, majeruhi saba wanaopata matibabu hali zao ni mbaya sana na wanahitaji uangalizi wa karibu zaidi. Madaktari wameendelea kutafuta namna za kitaalamu zaidi kuokoa maisha yao kutokana na majeraha makubwa ya moto waliyoyapata,” alisema.
Ofisa Habari Msaidizi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dorice Ishenda alisema waliofariki dunia hadi kufikia jana asubuhi ni Nurdin Mazinga (24) na Abbas Uganga (21) hivyo kufanya waliofariki dunia kufikia saba na majeruhi wengine tisa wakiendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo.
Alisema majeruhi wawili tu kati ya tisa, ambao hali zao angalau zinatia matumaini kutokana na kuweza kuzungumza na kutokuwa na majeraha makubwa ya kutisha.
Wengine waliopoteza maisha awali ni Mohamed Hassan (36), Hassan Ismail (19), Maulid Rajab (61) na Mohamed Ismail (21).
Idadi hiyo inafanya watu waliofariki dunia kutokana na ajali hiyo kufikia saba, akiwamo wa kwanza aliyefariki kwenye tukio hilo kabla ya kufikishwa hospitali.
Chanzo cha ajali
Chanzo cha ajali hiyo ni watu waliokuwa wakichota petroli iliyomwagika baada ya lori hilo kupinduka. Wachotaji hao walificha mafuta hayo kwenye nyumba za jirani na mlipuko huo ulipotokea moto ulifuata mafuta hayo na kuleta madhara kwenye eneo hilo.
Juzi Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk Amani Malima alisema walikuwa wamebaki majeruhi wanne.

15 Oktoba 2014

Trafiki watatu wafukuzwa kazi

JESHI la Polisi mkoani Kagera limewafukuza kazi askari wake watatu kwa kulifedhehesha jeshi hilo kutokana na kitendo cha kupiga picha inayowaonyesha wawili kati yao wakinyonyana ndimi wakiwa kazini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe, alisema kitendo kilichofanywa na askari hao kimeshusha hadhi ya jeshi.
Aliwataja askari hao waliofukuzwa ni F.7788 PC Mpaji Mwasumbi, G 2122 PC Fadhili Linga na WP.8898 Veronica Mdeme ambao wote ni wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Misenyi.
Alisema PC Mpaji na WP Veronica walipiga picha inayokwenda kinyume na maadili ya Jeshi la Polisi wakiwa kazini, huku PC Fadhili akiingia matatani kwa kuwapiga picha hiyo chafu askari wenzake na kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Kamanda Mwaibambe alisema picha hiyo ilianza kuonekana katika mitandao mbalimbali ya kijamii mapema wiki hii.
Alisema askari PC Fadhili alipiga picha hiyo mwaka 2012 kwa kutumia simu yake ya kiganjani na kuitunza, lakini wiki hii aliamua kuisambaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kitendo ambacho ni kinyume na kazi yake.
“Napenda kuthibitisha kuwa picha hii iliyoonekana kwenye mitandao ya kijamii ni picha halisi ambayo haijachakachuliwa kabisa.
“Maadili ya kijeshi yapo kisheria na askari wetu wanafundishwa namna ya kuishi katika maisha ya utumishi wa jeshi na si vinginevyo.
“Jeshi halikubaliani na vitendo hivi, ikitokea askari kwenda kinyume lazima achukuliwe hatua kali,” alisema Kamanda Mwaibambe.
Taarifa zaidi kutoka mkoani Kagera, zinaeleza baada ya kusambazwa kwa picha hiyo na kuonekana katika mitandao ya kijamii, WP Veronica alianguka ghafla na kupoteza fahamu kwa mshtuko wa tukio hilo.
Kutokana na hali hiyo, majirani waliokuwa karibu na nyumbani kwake walilazimika kumpatia msaada na kumkimbiza hospitali kwa matibabu, ambako aliruhusiwa juzi jioni kabla ya kutiwa mbaroni.
DAR ES SALAAM
Wakati hayo yakiendelea, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewahamisha askari wake, WP 5863 Quine na WP 3548 Koplo Maeda kutoka Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Ilala kwa kukiuka maadili ya kazi.
Taarifa ya ndani ya Oktoba 2, mwaka huu ya Kikosi cha Usalama Barabarani Makao Makuu Dar es Salaam iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, imesema askari hao walisimamisha gari dogo na baada ya dereva kujitetea, waliendelea kutafuta makosa hali iliyosababisha abiria aliyekuwa mgonjwa kufariki.
Kutokana na tukio hilo, makamanda wa polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Kipolisi wa Dar es Salaam wametakiwa kuwakumbusha askari wao kuepuka kutolazimisha kutafuta makosa ambayo hayana madhara.
“Makosa ambayo hayana madhara katika kusababisha ajali mfano ni vifaa vya kuzimia moto, rangi, kadi kutoandika anuani, motor vehicle, leseni chini ya siku 30 na kadhalika,” lilisomeka agizo hilo kwa makamanda hao wa polisi.

Lori la mafuta laleta maafa Dar

WATU wanne wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori lililokuwa limebeba mafuta ya petroli kuanguka na kuteketea kwa moto katika eneo la Mbagala Rangitatu.
Hali hiyo ilizua taharuki na vilio kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo jirani, baada ya idadi kubwa ya watu kujeruhiwa vibaya kutokana na moto huo ulioanza saa 6 usiku.
Watu wengi walijeruhiwa baada ya kwenda kuchota mafuta yaliyokuwa yanamwagika wakiwa na ndoo, vidumu vya lita tano na vyombo vingine bila kuchukua tahadhari.
Chanzo chetu kimepasha kuwa lori hilo aina ya Scania lenye namba T 347 BXG na tela T 464 CSR mali ya Kampuni ya MOIL ya Mwanza, lilikuwa limebeba lita 38,000 za mafuta ya petroli.
Wakizungumza na MTANZANIA jana asubuhi, mashuhuda waliokuwapo eneo la tukio walisema moto huo ulilipuka usiku wa kumkia jana, baada ya lori hilo kuanguka likiwa katika harakati za kukwepa gari jingine.
MTANZANIA lilishuhudia umati mkubwa wa watu ukiwa umelizunguka lori hilo ambalo lilikuwa limeteketea kwa moto pamoja na nyumba mbili zilizopo jirani.
Nyumba moja ambayo ilikuwa na maduka iliteketea yote wakati nyumba ya wageni ya United States iliungua baadhi ya sehemu.
Wakati MTANZANIA likiwa eneo hilo lilishuhudia moto ukiendelea kuwaka katika moja ya maduka yaliyokuwamo kwenye nyumba hiyo.
Wakati hali ikizidi kuwa tete, polisi waliimarisha ulinzi kwa kuzuia watu waliokuwa wamefurika eneo hilo wasisogelee tena lori hilo.
Mmoja wa mashuhuda, Bakari Seleman alisema tukio hilo lilitokea baada ya lori hilo kuanguka wakati dereva alipokuwa akijaribu kulikwepa gari jingine.
“Yule dereva wa lori alikuwa anajaribu kulikwepa gari jingine lililokuwa likitokea Kongowe ambalo liliingia ghafla barabarani,” alisema Seleman.
Alisema baada ya lori hilo kuanguka halikuleta madhara yoyote na kwamba dereva alitoka salama na kuwatahadharisha watu wasilisogelee.
“Dereva alikuwa amesimama kwenye kichuguu akawaaambia watu wasisogee kwa sababu gari limebeba mafuta ya petroli, lakini baada ya muda lilikuja kundi la vijana wakiwa na mifuko ya plastiki na madumu wakaanza kuchukua mafuta,” alisema.
CHANZO CHA MOTO
Shuhuda mwingine, alisema baadhi ya vijana walikuwa wakichota mafuta na kuyahifadhi katika nyumba ya kulala wageni iliyokuwa jirani.
Alisema moto huo ulianza kulipuka baada ya muuza chipsi katika nyumba hiyo ya kulala wageni kupita na dumu la mafuta jirani na jiko.
“Yule muuza chipsi alitoka kwenda kuchukua mafuta na wakati anarudi akapita na dumu palepale jikoni ndipo moto ukalipuka. Alianza kuungua sehemu mbalimbali za mwili wake, akawa anakimbilia kwenye vyumba.
“Kule kwenye vyumba ndiko kulikokuwa kumehifadhiwa madumu mengine, kwahiyo alipofika maeneo yale moto ukaongezeka zaidi kuwaka, akaungua vibaya na kupoteza maisha,” alisema.
Shuhuda mwingine ambaye ni mmoja wa wafanyakazi wa nyumba hiyo ya kulala wageni (aliomba asitajwe jina), alisema baadhi ya pikipiki na baiskeli zilizokuwa nje ya nyumba hiyo ziliteketea kwa moto.
“Hapa nje kulikuwa na pikipiki kama tisa hivi na baiskeli zimeteketea kabisa,” alisema shuhuda huyo.
KAULI YA POLISI
Akizungumza na MTANZANIA, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Nyigesa Wankyo, alisema katika ajali hiyo mtu mmoja alifariki na wengine 19 kujeruhiwa. Ingawa hadi jana jioni watu wanne walikuwa wamefariki.
Alimtaja marehemu kuwa ni Masoud Masoud mkazi wa Charambe na kati ya majeruhi, 18 ni wanaume na mwanamke mmoja.
Alisema chanzo cha ajali hiyo ni gari kuacha njia na kupinduka.
MGANGA MKUU
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk. Amani Malima, alisema alipokea maiti moja na majeruhi 21.
“Majeruhi 15 walihamishiwa Hospitali ya Muhimbili baada ya hali zao kuwa mbaya na sasa wamebaki majeruhi sita,” alisema Dk. Malima.
Alisema majeruhi hao wameungua sehemu mbalimbali za miili yao, zikiwamo za siri na usoni.
MUHIMBILI
Ofisa Uhusiano Msaidizi wa Hospitali ya Muhimbili, Dorice Ishenga, alisema kati ya majeruhi waliofikishwa hospitalini hapo, watatu walifariki dunia na wengine wanaendelea kupatiwa matibabu.
“Wamebaki majeruhi 12 madaktari wanaendelea kupambana ili kuokoa maisha yao,” alisema Ishenga.
Matukio ya aina hii yameripotiwa kutokea mara kadhaa nchini. Mwaka 2007, watu kadhaa walipoteza maisha kwa ajali ya moto walipokuwa wakichota mafuta mkoani Mbeya.
Februari 5, mwaka huu lori la mafuta lililipuka eneo la Mlima Sekenke mkoani Singida ambapo watu wanane walifariki dunia wakichota mafuta.
Nchini Kenya, zaidi ya watu 90 waliokuwa wakichota mafuta kutoka kwenye lori la mafuta lililopinduka katika mji wa Molo walifariki dunia kwa kuungua vibaya mwaka 2000.

14 Oktoba 2014

Mwanafunzi chuo kikuu alazimishwa kurekodi picha za ngono

Kweli dunia ina mambo! Kuna watu wanajaribu kutumia kila fursa inayopatikana kujinufaisha kwa kupata fedha hata ziwe ‘chafu’, kwao kitu cha maana ni kupata utajiri kwanza.

Kundi la watu wanaofanya biashara ya kusafirisha watu, wamekuwa wakitumia fursa ya ukosefu wa ajira kama chambo cha kuwanasa vijana na kuwaingiza kwenye biashara haramu kama ukahaba.

Hivi karibu kundi hilo linalosafirisha watu lilipita katika vyuo vikuu kadhaa nchini Uganda na kuwaahidi wanafunzi kuwa lingewatafutia kazi Ulaya na Marekani, kwani lina uzoefu wa kutosha na kazi hiyo.

 Mmoja wa vijana ‘waliobahatika’ kupata nafasi ya kwenda Ulaya kufanya kazi ni Sunday Bekunda (25), mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu cha Makerere, Kampala.

Kwa bahati mbaya ‘neema’ ya kwenda Ulaya iligeuka balaa baada ya kutekwa na kulazimishwa kufanya ngono na wanawake mbalimbali huku akirekodiwa kwenye kamera za video.

“Ilikuwa ni Januari 2013, nilipokutana na mwanaume mmoja anayeitwa Charles kutoka katikati ya Jiji la Kampala, ambaye aliniahidi kunipeleka Kenya kufanya kazi katika kiwanda.

“Sikujua kuwa Charles alikuwa msafirisha watu. Alikuwa anaonekana kama mzazi wa makamo aliyefanya kazi kwa miaka mingi.

“Nilifungua moyo wangu na kumweleza changamoto nyingi ninazopitia na namna nilivyo hangaika kutafuta kazi ili nipate fedha za kulipia masomo ya ziada. Kwa kifupi ni kama nilikuwa namwambia Charles kuwa sikuwa natafuta kazi bali nilikuwa nataka kazi yoyote.”

Safari ya Kenya

“Siku iliyofuata nilikuwa tayari kwa safari na nilimkuta Charles akiwa kwenye gari la binafsi aina ya Toyota Noah. Alikuwa pamoja na wasichana sita na wavulana wawili. Alituambia kuwa tutaingia Kenya kwa kupitia mpaka usio rasmi unaoitwa Chepskunya.

“Tukiwa njiani, Charles alikuwa anaongea sana na kutusisitizia kuwa ‘tusimwangushe’ tukifika huko. “Tulipofika Kenya walituchukua na kutuingiza kwenye nyumba moja nzuri ya makazi ya watu, hapo tulikutana na wenzetu 15, wavulana wawili kutoka Rwanda na Wakenya 13.”

Kutekwa

“Charles alituacha hapo tukiwa chini ya mwanamke mmoja na wanaume wanne wenye miili iliyojengeka vyema. Watu hao walianza kutupiga makofi na kutulazimisha tuvue nguo. Ndipo nilipobaini kuwa kilichoonekana kama ni safari sasa imegeuka utekaji.

11 Oktoba 2014

HAWAFAI KABISA: Lampard akoshwa na Costa, Fabregas

FRANK Lampard hayupo ndani ya kikosi cha Chelsea kwa mara ya kwanza baada ya miaka 13. Siku hizi anavaa jezi ya Manchester City. Lakini bado anatupa jicho la umbea katika timu yake ya zamani na anakwambia Cesc Fabregas na Diego Costa hawafai hata kidogo!
Chelsea imetumia zaidi ya Pauni 100 milioni kuwachukua Filipe Luis, Cesc Fabregas, Diego Costa, Didier Drogba na Loic Remy na imewaruhusu Ashley Cole, David Luiz, Samuel Eto’o na yeye kuondoka Stamford.
Lakini Lampard ameonyesha kukoshwa vilivyo na viwango vinavyoonyeshwa na Costa na Fabregas ambao pia ni nyota wa kimataifa wa Hispania.
Nyota hao wameonyesha maelewano makubwa uwanjani na kuweika Chelsea kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa na pointi 19 huku wakiwa hawajapoteza mechi.
“Nimetazama mechi zao tokea mbali na pia nimecheza dhidi yao. Hakuna yeyote kati yao ambaye amenishangaza. Cesc Fabregas nimecheza dhidi yake akiwa Arsenal. Anaijua Ligi Kuu ya England na ni mchezaji wa kiwango cha dunia,” alisema Lampard.
“Tulimtazama Diego Costa kabla hatujacheza na Atletico Madrid pambano la nusu fainali Ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu uliopita. Tulitazama video zake na tungeweza kutazama hata kwa saa tatu jinsi alivyokuwa anakimbia, jinsi alivyokuwa anafunga mabao na kila kitu alichokuwa anakifanya uwanjani. Niliona kuwa alikuwa bonge la mchezaji na Chelsea hatimaye ilimsajili,” aliongeza Lampard.
Tayari Costa ameivamia kwa fujo Ligi Kuu ya England huku akiwa amefunga mabao tisa kufuatia uhamisho wake wa Pauni 32 milioni kutoka Atletico Madrid ambayo aliipatia ubingwa wa La Liga msimu uliopita huku pia akiifikisha fainali za Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.
Wakati huo huo, Fabregas amepiga pasi saba za mabao huku pasi moja akiipika katika bao la pili la ushindi la Costa dhidi ya timu yake ya zamani, Arsenal Jumapili iliyopita katika Uwanja wa Stamford Bridge.
Wengi wanatabiri kuwa, Fabregas atachukua umuhimu wa Lampard katika kikosi cha Kocha Jose Mourinho ingawa Lampard anakumbukwa kwa kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Chelsea akiwa na mabao 211 katika kikosi hicho.

09 Oktoba 2014

Madini ya Sh15.8 bilioni yakamatwa yakitoroshwa

Chalinze. Wakala wa Ukaguzi wa Madini nchini (TMAA), umekamata madini yenye thamani ya Sh15.8 bilioni yaliyokuwa yakitoroshwa kwenda nje ya nchi bila ya kibali na kukwepa kulipa kodi ya mapato.
Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Uzalishaji na Biashara ya Madini wa TMAA, Conrad Mtui alisema kuwa kiasi hicho cha madini aina mbalimbali kilikamatwa kati ya Julai, 2012 hadi Agosti, mwaka huu.
Mtui aliwaambia waandishi wa habari juzi katika ziara ya kutembelea migodi ya madini ya ujenzi ya Lugoba na Msolwa wilayani Bagamoyo, kuwa wakala ulikamata madini hayo katika matukio 53 ambayo yaliwahusisha mawakala wa madini.
“Baada ya kuanzisha madawati ya ukaguzi kwenye viwanja vya Kimataifa vya Ndege vya Julius Nyerere (JNIA), Kilimanjaro na Mwanza, tuliwakamata wote waliokuwa wakijaribu kusafirisha madini hayo kinyume cha sheria, matukio haya yanaweza pia kuongezeka muda wowote.





“Wahusika wamefikishwa mahakamani na baadhi yao wamehukumiwa na madini yao kutaifishwa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010,” alisema Mtui.
Alipoulizwa kama kuna wachimbaji wakubwa waliokamatwa wakifanya hujuma hiyo, Mtui alisema waliokamatwa wengi walikuwa wafanyabiashara wadogo na madalali na hakukuwa na kampuni kubwa kwa kuwa kuna utaratibu maalumu wa ukaguzi na usafirishaji.
Hata hivyo, Mtui alisema baada ya kukaza uzi wa ukaguzi walifanikiwa kuongeza mrabaha kutoka kwenye migodi mikubwa ya dhahabu kiasi cha Dola za Marekani 427.98 kuanzia mwaka 2005 hadi mwishoni mwa Agosti mwaka huu.
“Wakala ulifanya ukaguzi na uhakiki wa madini yaliyozalishwa na kuuzwa na migodi mikubwa nchini. Ukaguzi huo ulisaidia kujua kiasi na thamani halisi ya madini yaliyozalishwa na kuuzwa kutoka migodi mbalimbali, ikiwamo saba ya dhahabu ya Geita, Golden Pride, Bulyanhulu, Tulawaka, North Mara, Buzwagi na New Luika,” alisema.
Pamoja na kujinadi kwa mafanikio hayo, Mtui alisema bado kuna ujanja wa utoroshaji kupitia njia za panya na upungufu wa rasilimali watu unawazuia kufanya ukaguzi katika migodi midogo, hivyo kuchangia upotevu wa mapato.
“Tuna wakaguzi wetu katika baadhi ya migodi midogo yenye uzalishaji mkubwa...lakini kwa mingine ni hasara kwa sababu unaweza kukuta malipo ya wakaguzi ni makubwa kuliko mrabaha unaopatikana,” alisema.

Wanafunzi Njombe wateketeza bweni

Njombe. Shule ya Sekondari ya Wavulana Njombe (Njoss) iliyoko mjini hapa, imefungwa kuanzia jana hadi Novemba 8, mwaka huu, baada ya wanafunzi kuchoma moto bweni, karakana na kuharibu mali mbalimbali za shule na walimu.
Wanafunzi hao wanadaiwa pia kuharibu majengo ya Shule ya Msingi Kilimani iliyo karibu na shule hiyo.
Uamuzi wa kuifunga shule ulitolewa jana na Ofisa Elimu wa Mkoa wa Njombe, Said Nyasiro baada ya kufika katika eneo la tukio akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sarah Dumba na Ofisa Elimu wa Shule za Sekondari wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Venance Msungu na kufanya kikao cha ndani na walimu.


Nyasiro aliagiza kila mwanafunzi arudipo shuleni hapo, aende na Sh 150,000 kwa ajili ya kufidia hasara iliyopatikana na wanafunzi wote 1,000, waambatane na wazazi wao. Tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kuamkia jana.
Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kwa zaidi ya saa mbili ili kuwatuliza, huku wakazi wanaoishi jirani na shule wakiwa wamejawa hofu kutokana na milio ya mabomu iliyokuwa ikirindima.
Polisi waliokuwa katika eneo la tukio, walisema hali ingekuwa mbaya zaidi kama wasingewahi kufika.
Mbali ya kuchoma moto bweni na karakana, walianza kuvamia nyumba za walimu na kuharibu mali zao.
Inadaiwa kuwa walichoma pia gari la mwalimu wa taaluma ambaye jina lake halikufahamika mara moja na kisha kuvunja duka lake na kuharibu vitu mbalimbali kabla ya kuvamia nyumba ya mkuu wa shule, Bernard William na kuvunja vioo vya madirisha.
Inadaiwa wanafunzi hao walifikia hatua hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutaka kuushinikiza uongozi wa shule uwarudishe wenzao 30 waliosimamishwa masomo kutokana na utovu wa nidhamu.
Mkuu wa shule hiyo, William alisema bweni hilo lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 102, limeteketea lote na mali zilizokuwamo ndani. Alisema uharibifu huo unawaongezea gharama nyingine ya ukarabati kwani wakati tukio hilo linatokea, shule ilikuwa inafanya ukarabati wa bweni lingine lililoungua moto hivi karibuni.
Alisema chanzo cha wanafunzi kufikia uamuzi huo ni kudai kuonewa kwa wenzao 30 waliosimamishwa masomo kutokana na utovu wa nidhamu, ambapo 29 kati ya hao wanakabiliwa na kosa la kutoroka na kwenda kufanya fujo kwenye disko lililokuwa likipigwa Chuo cha Maendeleo, Njombe.
Mwalimu William alisema mwanafunzi mmoja amesimamishwa kwa kosa la kukutwa na simu darasani wakati sheria za shule haziruhusu.

05 Oktoba 2014

Wenger:Costa ni moto wa kuotea mbali


Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa Diego Costa ni mshambuliaji hatari na kwamba mshambuliaji huyo wa Chelsea ni tishio kubwa kwa kikosi chake katika mechi ya Leo itakayochezwa katika uga wa stamford Bridge.
Kilabu zote mbili hazijafungwa tangu msimu huu wa ligi uanze,lakini Chelsea iko juu ya Arsenal kwa pointi sita.
Costa aliyenunuliwa kwa kitita cha pauni millioni 32 kutoka kilabu ya Uhispania ya Atletico Madrid,amefunga mabao 8 katika mechi 6 za ligi ya Uingereza alizoshiriki.


''Costa ana kila kitu cha mshambuliaji,anajitolea na yuko tayari kufunga bao'',alisema Wenger.
Wenger anahisi matumaini kwamba huenda Arsenal ikaishangaza Chelsea ilio katika kilele cha jedwali la ligi ya Uingereza ikiwa na pointi 16 kati ya 18.
Msimu uliopita Arsenal ilipata kichapo cha mabao 6 kwa 0 katika mechi iliochezwa katika uga wa Stanford Bridge huku Wenger akiweka rekodi ya kuisimamia kilabu hiyo kwa mechi yake ya1000.
Kwa upande wake Mourinho anatarajia ushindani mkali kutoka kwa Arsenal na amejitayarisha vilivyo.

Adventist World Magazine

Why are many church choirs dying?

Diamond atwaa tuzo ya Mtv-Base

NYOTA ya Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini, Nassib Abdul ‘Diamond’, imezidi kung’aa baada ya kutwaa tuzo ya Msanii Bora wa mwezi huu wa Kituo cha Televisheni cha Mtv-Base cha Afrika Kusini.
Mbali na kutwaa tuzo hiyo, Diamond pia anawania tuzo ya All African Music (Afrima) inayofanyika nchini Nigeria pamoja na wasanii wenzake Peter Msechu na Vanessa Mdee.
Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa televisheni hiyo, zilieleza kwamba kila mwezi wanakuwa na tuzo hiyo ambapo inatokana na vipindi vyao mbalimbali kama Mixtape na 10 Bora.
Ilieleza mashabiki hupiga kura kupitia mitandao ya kijamii ambapo huulizwa na nyimbo zipi ambazo zinapigwa kwa mwezi husika na mwisho wa siku hupata mshindi.
Katika tuzo hizo za Afrima, Vanessa anawania vipengele viwili vikiwemo vya Msanii Bora Afrika Mashariki pamoja na Msanii Bora Afrika wa miondoko ya R&B Soul.
Diamond na Msechu wametajwa kuwania tuzo ya Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki pamoja na Wimbo Bora wa kushirikiana.
Wasanii waliotajwa kuwania tuzo hizo, watawasilisha kazi zao kwa jopo la majaji wa Afrima kwa nyimbo zao walizotoa kati ya Mei 15, mwaka jana hadi Julai 21, mwaka huu na kwamba jumla ya kazi 2,025 zilipokelewa kufanyiwa kazi.

Ugonjwa wa hemoroid (haenorrhoids)

Hemoroid ni ugonjwa unaoujulikana pia kama ugonjwa wa vifundo katika njia ya haja kubwa. Hata hivyo, huwa na majina mengi kama bawasili ukisababishwa na kulegea kwa misuli laini ya mishipa hiyo ya damu, hivyo mishipa husika hutanuka kuliko kawaida na kulegea, kisha kutokeza katika njia ya haja kubwa ikiambatana na ukuta wa njia hiyo. Sababu hasa ya kulegea kwa mishipa hiyo hazijaweza kueleweka.

Lakini, mabadiliko yafuatayo huchangia kwa kiasi kikubwa mtu kupatwa na hemoroid nayo ni; kupata choo kigumu mara kwa mara, kuharisha mara kwa mara, kukaa kwa muda mrefu, kuwa na uzito mkubwa kuliko inavyotakiwa (BMI>30), kukohoa mara kwa mara, uvimbe tumboni, kuzaa watoto wenye uzito mkubwa mfano zaidi ya kilo nne.

Baadhi ya dalili za ugonjwa huu ni kuhisi kushuka kwa fundo la sehemu ya haja kubwa wakati wa kupata choo, ambalo linaweza kurudi lenyewe ndani baada ya kupata choo, au inabidi kulirudisha kwa kidole, au kushindikana kabisa kurudishwa kwa kidole na kubaki likininng’inia nje kwa muda mrefu.

Nyingine ni kutokwa damu wakati wa haja kubwa inayoweza kuchafua nguo za ndani, wakati mwingine damu hutoka kwa wingi na mfululizo bila kuganda, hvyo uhatarisha maisha.

Uchunguzi na matibabu

Vipimo kama proctoscopy (kuchuguza kwa chombo maalumu chenye mwanga), proctosigmoidoscopy huweza kufanyika, pia kuwekewa dawa maalumu, kisha kupiga ex-ray (barium enema). Kwa watu walio na umri mkubwa, mfano zaidi ya miaka 50 ni muhimu zaidi kuchunguzwa kitaalamu kwani hilo ni kundi lililo kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya njia ya haja kubwa. Mtu anaweza kufikiri ni tatizo dogo, kumbe anasumbuliwa na saratani ya njia ya haja kubwa, hivyo matibabu hubadilika.

Matibabu

Iwapo hemoroids hazijawa kubwa, yaani zipo katika hatua ya kwanza au ya pili ni muhimu kutibu vinavyochochea ugonjwa kama vilivyoainishwa hapo juu. Iwapo tatizo lipo katika hatua ya tatu au ya nne, au matibabu tajwa hapo juu yameshindikana, upasuaji ndiyo matibabu sahihi ya ugonjwa huu.

PINDA AMPINGA KIKWETE

SIKU chache baada ya Bunge Maalum la Katiba kupitisha kwa mbinde katiba inayopendekezwa, Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwapo kwa mpasuko mpya ndani ya Chama. Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali.

Mpasuko huo umewagawa makada wa CCM katika makundi mawili, moja likitaka kura ya maoni juu ya Katiba ifanywe kabla ya uchaguzi mkuu ujao huku jingine likitaka ifanyike baada ya Uchaguzi Mkuu.

Kundi linalopinga linataka kuheshimiwa kwa mazungumzo kati ya Rais Kikwete na viongozi wa vyama vya siasa kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) waliokubaliana kura za maoni zifanyike mwaka 2016.

Katika kikao hicho kilichofanyika mwezi uliopita, Rais Kikwete na wapinzani walikubaliana Bunge la Katiba liishie Oktoba 4 mwaka huu, na Rasimu ya Katiba isipelekwe kwa wananchi kupigiwa kura ya maoni.

Ilipendekezwa kwenye kikao hicho yafanyike marekebisho katika katiba ya sasa ili kuingiza vipengele vya tume huru ya uchaguzi, mgombea binafsi, matokeo ya Rais kupingwa mahakamani na mshindi wa urais kupata kura zaidi ya asilimia 50.

Kwa makubaliano hayo, mchakato wa kura ya maoni kama utakuwepo, utaamriwa na rais ajaye ikiwa atataka kuanzia pale mchakato huo ulipoishia au kuanzia pale ilipoishia Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Uamuzi huo ulikuwa pigo kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta, aliyetutumua kuwa Oktoba 31 mwaka huu wangemkabidhi Rais Kikwete katiba inayopendekezwa.

Hata hivyo, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa kuwa baadhi ya vigogo wa CCM akiwemo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, anayetajwa kutaka kuwania urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani, wanataka kura za maoni zifanyike chini ya utawala wa sasa.

Inadaiwa kundi hilo linataka jambo hilo lifanyike sasa ili rais ajaye asibebeshwe mzigo ambao hakuuanzisha.

Kauli kama hiyo ilitolewa na Pinda siku ya kuvunjwa Bunge akisema angependa mchakato wa kura za maoni ufanywe pamoja na uchaguzi mkuu wa mwakani.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wamelidokezwa Tanzania Daima Jumapili kuwa kauli ya Pinda ni sawa na kumshauri Rais Kikwete, atupilie mbali makubaliano yake na vyama vya siasa

Ushauri huo umezua maswali mengi kuhusu ajenda iliyo nyuma yake, na kwamba utamuathiri zaidi Rais Kikwete iwapo ataukubali.

Inaelezwa kama Rais Kikwete akiukubali ataonekana ataonekana ni asiye na msimamo katika mambo ya msingi, anayeweza kubadilika kwa ushauri kinzani wa wasaidizi wake.

Katika hatua ya kushangaza, katika salamu zake kwa wajumbe muda mfupi kabla Bunge halijavunjwa, Pinda alisema angependa kuona mchakato huo unakamilika kabla Rais Kikwete hajaondoka.

“Maana unaweza kuachia jambo hili kwa nia njema tu lakini wengine wakafikiri umeliacha ili kuendeleza vurugu. Tujitahidi kuona kama hili jambo litakwenda hadi mwisho.

“Nashauri hata kama ikiwezekana kwenda kwenye uchaguzi mkuu mwaka kesho tukiwa na kura mbili za kumtafuta Rais na ile ya maoni ya katiba bora tulimalize,” alisema Pinda.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa kuwa ndani ya CCM kuna makundi mawili ambayo yanasigana kuhusu mchakato huo ama umalizwe na Kikwete mwenyewe au ungoje Rais ajaye.

Duru za kisiasa zinasema kuwa kwa jinsi mchakato huo ulivyovurugwa hasa na Bunge Maalumu chini ya Sitta, hakuna Rais ajaye anayeweza kukubali katiba inayopendekezwa iende kwa wananchi kupigiwa kura wakati inaonekana dhahiri imetawaliwa na mizengwe na imekataliwa tangu ikiwa bungeni.

“Hoja hii ya Pinda ndio mtazamo wa wagombea urais wengi ndani ya CCM wanavyotaka Rais Kikwete abebe msalaba wake kwa kumaliza mchakato wake aliyouasisi kuliko kuja kumbebesha mrithi wake,”kilisema chanzo chetu.

Kundi linalounga mkono kura za maoni kufanyika mwaka 2016, lina imani Rais ajaye atakuwa amepata fundisho kubwa kupitia mchakato wa sasa na hivyo atataka kwanza yafanyike maridhiano ya kuamua suala la muundo wa muungano.

Msigiano wa pande hizo mbili umezua mpasuko mpya unaonekana kulenga urais wa mwaka 2015.




Takwimu zaleta utata

Takwimu za kukinzana zilizotolewa na Sitta kuhusu idadi ya wajumbe wa Bunge hilo waliotakiwa kupiga kura ya kupitisha rasimu ya katiba inayopendekezwa, zimevuruga ukokotoaji wa theluthi mbili na hivyo kuibua tuhuma za uchakachuaji.

Muda mfupi kabla ya upigaji kura kuanza, Sitta alilieleza Bunge kuwa idadi ya wajumbe ilikuwa 630 lakini baada ya kifo cha mjumbe, Shida Salum, wamebaki 629 ambapo kati yao 130 ni wajumbe wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) waliosusia.

Kwa mujibu wa Sitta, katika idadi hiyo wajumbe wa Bara ni 419 na Zanzibar ni 210, na kwamba ili kupata theluthi mbili ya kura za Bara lazima wawe na wajumbe 280 wanaunga mkono wakati kwa Zanzibar wanatakiwa wajumbe 140.

Hizi ndizo takwimu walizokuwa wakitumia wajumbe wa Ukawa kukokotoa theluthi mbili ya Zanzibar na kujiridhisha kwamba kwa idadi ya wajumbe 67 walionao Zanzibar, rasimu ya katiba inayopendekezwa isingepitishwa.

Wajumbe 67 wa Ukawa kutoka Zanzibar wakijumlishwa na wajumbe saba wa kundi la 201 kutoka Zanzibar waliopiga kura ya ‘hapana’ wanafikia 74 na ukiongeza wajumbe watatu yaani Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Abdallah Abas na Ali Omar Juma waliopiga kura za hapana katika ibara nyingi kura za hapana zingefika 77.

Kwa maana hiyo, Ukawa walichukua 210 wakatoa 74 wakapata 136, idadi ambayo haikidhi akidi au 133 ukitoa kwa wajumbe 77, na hivyo wakajihalalishia ushindi bila kutegemea majaaliwa ya wajumbe waliopiga kura za siri kama kungetokea ambao wangepiga ‘hapana’.

Lakini katika hatua ya kushangaza, siku ya kutangaza matokeo takwimu hizo zilibadilika, ambapo, Naibu Katibu wa Bunge Maalum, Dk. Thomas Kashililah, alisema idadi ya wajumbe ni 630, wajumbe 219 ni kutoka Zanzibar na Bara ni 411.

Kwamba kati ya hao, waliopiga kura kwa upande wa Zanzibar ni 154 na ili kupata theluthi mbili ya huko zilihitajika kura za wajumbe 146 wakati theluthi mbili kwa upande wa Bara ilitakiwa kuwa wajumbe 274.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, tayari hesabu ya Ukawa ilikuwa imevurugika kwani taarifa za Bunge zilisema kuwa wajumbe wote 31 wa Zanzibar waliopiga kura ya siri, walipiga ‘ndiyo’.

Dk. Kashililah alisema kuwa theluthi mbili ya Zanzibar ilipatikana kwa ibara zote 289 ambapo ilikuwa ikibadilika kati ya 146, 147 na 148 wakati kwa upande wa Bara theluthi mbili ilikuwa ikibadilika kuanzia 332, 333 na 334 kutegemeana na ibara.

“Kwa upande wa Zanzibar, wajumbe waliopiga kura za ndiyo za wazi ni kati ya 106 hadi 108, wajumbe kati ya 7 hadi 8 walipiga kura za hapana za wazi wakati kura za siri zilikuwa kati ya 38 hadi 40 ambazo zote zilikuwa za ndiyo isipokuwa moja tu ilikuwa ya hapana katika baadhi ya ibara,” alisema.

Kwa Bara, kura za ndiyo za wazi zilikuwa kati ya 301 na 304, kura ya wazi ya hapana ilikuwa kati ya moja na tatu. Kura za siri za ndiyo zilikuwa kati ya 29 na 31 wakati kura za siri za hapana zilikuwa kati ya moja na mbili.

Hali hiyo ndiyo imeacha maswali mengi kuhusiana na upatikanaji wa theluthi mbili ya Zanzibar hasa baada ya baadhi ya wajumbe kudai kurubuniwa kwa fedha ili wapige kura ya ndiyo.

Sitta aliongeza utata pale alipolitangazia Bunge wakati kura zikiendelea kuhesabiwa kuwa wajumbe wawili wa Ukawa kutoka Zanzibar walikubali kupiga kura ya ndiyo wakati awali alishasema kuwa kura za Ukawa zingehesabika kama za hapana kwasababu hawakushiriki mchakato huo.

Uamuzi wa Sitta uliwashtua hata wajumbe wa CCM ambao baadhi walihoji inawezekanaje mjumbe ambaye hakushiriki mijadala kwa makusudi aruhusiwe kupiga kura, tena akiwa nje ya Bunge.

Sitta alitamba akisema kuwa, “baada ya tangazo langu kwamba wale wote walioko nje watapiga kura, wajumbe wawili ambao walikuwa kwenye ule mgomo wa kile kiukundi cha Ukawa wameisoma katiba inayopendekezwa wakaona ni kitu cha kizalendo kuipigia kura.”

Sitta alisema kuwa wajumbe hao ambao ni kutoka Zanzibar, na mmoja wao yuko radhi kufukuzwa hata uanachama wa chama chake baada ya kupiga kura, ingawa hawakuwa katika orodha ya wale waliotangazwa kuwa walipata ruhusa ya mwenyekiti kupiga kura wakiwa nje ya Bunge kwa sababu maalumu.
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728