28 Desemba 2015

Stoke City, Spurs washinda mechi muhimu

Joselu 
Siku chache baada ya kulaza Manchester United, Stoke City wameandikisha ushindi muhimu Ligi ya Uingereza kwa kucharaza Everton.

Carrick: Tunacheza kwa ajili ya Van Gaal

Man UtdNahodha msaidizi wa Manchester United, Michael Carrick amelalamika madai kuwa wachezaji wa klabu hiyo hawachezi vizuri ili kulinda kibarua cha kocha wao.

LVG: Naweza kuondoka mwenyewe Man United

 
Kocha wa Manchester United Louis van Gaal amesema kuwa anaweza "kujiuzulu mwenyewe" baada ya Stoke City kuwapiga magoli 2-0 katika kichapo chao cha nne mfululizo katika michuano yote.

CCM: Jiwekeni tayari kwa uchaguzi Zanzibar

Samia 
Chama cha Mapinduzi kimewataka wanachama wake visiwani Zanzibar kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi.
Tamko hilo limetolewa huku mazungumzo hakiendelea kutafuta suluhu ya mzozo kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 ambayo yalifutiliwa mbali.
Wito wa wafuasi kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi ume

Kizingiti mazungumzo ya amani Burundi

Januari 
Mazungumzo ya kujaribu kutafutia ufumbuzi mzozo wa kisiasa nchini Burundi yamefanyika nchini Uganda.
Hata hivyo washiriki wamekosa kuelewana kuhusu siku ya kuanza kwa mazungumzo kamili.

Wapiganaji waondolewa Syria

Hezbollah 
Wapiganaji wa makundi ya waasi Syria wameanza kuondolewa kutoka mji wa Zabadani karibu na mpaka wa Syria na Lebanon.

Mbwa aliyeuawa Paris kupewa nishani ya ushujaa

Diesel 
Mbwa wa polisi aliyeuawa wakati wa msako baada ya mashambulio ya Paris atatunukiwa nishani kuu ya ushujaa.

Mlinzi wa Osama bin Laden afariki dunia


Bahri
Taarifa kutoka Yemen zinasema aliyekuwa mlinzi wa Osama Bin Laden, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

20 Desemba 2015

Sanders aomba msamaha kumdukua Hillary Clinton

 Image caption Sanders aomba msamaha kumdukua Hillary Clinton
Mgombea anayewania tikiti ya chama cha Democratic nchini Marekani Bernie Sanders amekiri na kuomba msamaha kwa aliyekuwa waziri wa mashauri ya kigeni na pia mgombea mwenza
Bi Hillary Clinton kwa kudukua taarifa za upigaji kura, zilizo tayarishwa na kikosi cha kumfanyia kampeini Bi Clinton.

Tishio la 'Bomu' lalazimu ndege ya Ufaransa kutua Kenya

Image copyright AP
Image caption Wataalamu hao wanatoka kikosi cha jeshi la wanamaji wa Kenya na idara ya polisi wa upelelezi.
Ndege moja ya abiria ya Air France Boeing 777 AF463, inayohudumu kati ya Mauritius na Paris imelazimika kutua kwa ghafla katika uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Mombasa - Kenya baada ya kifaa kinachodhaniwa kuwa bomu kupatikana ndani ya choo cha ndege hiyo.

Gavana aomba msaada wa rais kupitia Facebook

Image copyright EPA
Image caption Afisa huyo Mohammad Jan Rasoulyar alimwandikia rais Ashraf Ghani kumweleza kuwa wanajeshi 90 wameuawa katika mapigano makali na wanamgambo wa Taliban
Naibu gavana wa jimbo la Helmand Kusini mwa Afghanistan amewashangaza wengi kwa kumuandikia rais wa Afghanistan barua kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook.

Utafiti: Hakuna ugaidi wa kadri au wenye misimamo mikali

Image copyright AP
Image caption Utafiti: Hakuna ugaidi wa kadri au wenye misimamo mikali
Thuluthi moja ya wapiganaji nchini Syria takriban wapiganaji laki moja wanaiunga mkono kundi la wapiganaji wa kiislamu wa Islamic State.
Utafiti mpya umebaini kuwa hata kundi la

17 Desemba 2015

Vyakula vya kiasili: Matoke


Vyakula vya nyumbani vinapendwa na watu wengi wanaoishi mataifa ya nje na ni moja ya biashara inayoleta faida kwa wanaoifanya.
Wengine wanasema wakila chakula cha nyumbani huwa wanakumbuka mengi na kujiona kama wako walikotoka.
Sikiliza makala hii ya Omar Mutasa kutoka Afrika kusini

16 Desemba 2015

Mshukiwa akamatwa kuhusu mauaji ya Paris

ParisImage copyrightAFP
Image captionWatu 130 waliuawa kwenye mashambulio ya Paris Novemba 13
Polisi nchini Ufaransa wamemkamata mwanamume eneo la Paris kwenye uchunguzi wao kuhusu mashambulio ya Novemba 13.

Taarifa kutoka Zanzibar

Taarifa kutoka Zanzibar zinasema boti ya Royal Express iliyokuwa imebeba abiria 367 ikitokea Unguja kuelekea kisiwa cha Pemba imeshika moto ikiwa njiani baada ya injini yake moja kupata

Fabregas: Wachezaji wacheze sawa na mishahara

ChelseaImage copyrightEPA
Image captionChelsea wamo nambari 16 ligini wakiwa na alama 15
Kiungo wa kati wa Chelsea amesema wachezaji wa Chelsea wanaolipwa mishahara mikubwa wanafaa kucheza kama wachezaji nyota.

Magufuli amfuta mkuu wa kupambana na rushwa

MagufuliImage copyrightStatehouse Tanzania
Image captionMagufuli amesema hajaridhishwa na utendakazi wa mkuu huyo
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Dkt Edward Hoseah, na pia akawasimamisha kazi maafisa wa nne wa taasisi hiyo.

Marekani yapandisha riba baada ya miaka 7

Image copyright
Image captionJanet Yellen Gavana wa Benki Kuu ya Marekani
Benki Kuu ya Marekani imepandisha kiwango kikuu cha riba kwa alama ya robo ya asilimia.

Ripoti mpya ya UNICEF yashtua

Image copyrightReuters
Image captionMiongoni mwa watoto wanaozaliwa katika maeneo yenye vita wakiwa na mama zao.
Zaidi ya watoto milioni 16 duniani, wamezaliwa katika mazingira ya kivita katika kipindi cha mwaka mmoja pekee.

Kanisa kuandaa ibada ya Star Wars

Star WarsImage copyrightl
Image captionFIlamu ya The Force Awakens imezua msisimko mkubwa kote duniani
Kanisa moja mjini Berlin limetangaza kwamba litaandaa ibada maalum kabla ya Krismasi itakayoongozwa na filamu ya Star Wars.

Yanga yapaa kileleni ligi ya Tanzania

Image captionTimu ya Yanga ya Tanzania
Timu ya soka ya Yanga imerejea tena kileleni mwa ligi ya Tanzania baada kupata ushindi dhidi ya African Sport.

TP Mazembe washindwa tena Japan

MazembeImage copyrightGetty
Image captionTP Mazembe walikuwa wamechapwa 3-0 robofainali
Mabingwa wa soka Afrika TP Mazembe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamecharazwa 2-1 na Club America ya Mexico katika michuano ya fainali za Kombe la Dunia la Klabu.

15 Desemba 2015

Utafiti: Uongozi ni ‘hatari kwa maisha

ShinikizoImage copyrightAFP
Image captionShinikizo kutokana na majukumu ya uongozi huenda vinaathiri afya ya viongozi
Utafiti uliofanyiwa afya ya viongozi wa mataifa mbalimbali umebaini huwa wanazeeka haraka na kupoteza miaka mitatu katika muda wao wa kuishi kwa sababu ya uongozi.

Shule zote Los Angeles zafungwa ghafla

Image copyrightCBS
Image captionShule zote Los Angels zafungwa ghafla
Shule zote za uma katika jimbo Los Angeles Marekani zimefungwa mara moja kufuatia tishio la usalama.

Mourinho: Naona aibu

Image copyrightGetty
Image captionNaona aibu baada ya kushindwa tena
Siku moja baada ya kuambulia kichapo cha 2-1 dhidi ya Leicester City , mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho sasa anadai wachezaji wanamsaliti

Leicester waadhibu Chelsea na kurudi kileleni

ChelseaImage copyrightGetty
Image captionWachezaji wa Leicester City wakisherehekea ushindi dhidi ya Chelsea
Mabingwa watetezi wa ligi kuu England Chelsea wamezidi kutumbukia kwenye matatizo baada ya kupokezwa kichapo cha 2-1 na Leicester City.

Ronaldo, Muller wamo kikosi bora Uefa

Image copyrightPA
Image captionThomas Muller
Kikosi bora cha wachezaji kumi na moja kilichocheza hatua ya makundi ya michuno ya klabu bingwa ulaya kimetangazwa na Uefa.

Makaburi matatu kuwekwa wi-fi Moscow

Chekhov
Image captionMwandishi mashuhuri Anton Chekhov ni mmoja wa watu mashuhuri waliozikwa Novodevichy
Makaburi matatu yanayotembelewa sana na watu jijini Moscow yatawekewa huduma ya mtandao ya wi-fi.

Mahakama yaagiza dawa ya Nurofen isiuzwe

Image copyrightReuters
Image captionMahakama yaagiza dawa ya Nurofen isiuzwe
Mahakama moja nchini Australia imepiga marufuku uuzaji wa dawa ya kichwa iitwayo Nurofen.

10 Desemba 2015

Uamsho warejeshwa mahakamani Zanzibar

Mahakama Kuu ya Zanzibar imewaita tena viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu ambao wanakabiliwa na kesi ya ugaidi katika mahakama za Tanzania Bara kusikiliza rufaa ya dhamana yao kwa kesi nyengine.
Baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu wakiwa kwenye mikutano yao visiwani Zanzibar.
Baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu wakiwa kwenye mikutano yao visiwani Zanzibar.
Mwandishi wetu aliye visiwani Zanzibar anasema vikosi vya ulinzi na usalama vimezingira maeneo yote ya Mahakama Kuu ya Vuga na hakuna aliyeruhusiwa kuingia ndani kusikiliza kinachoendelea. Kwa mengi zaidi sikiliza matangazo yetu ya mchana.

Mbwa wa Benjamin Netanyahu huuma wageni

KerryImage copyrightReuters
Image captionKaiya amewahi kukutanishwa na John Kerry
Mbwa ambaye anayefugwa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliwauma wageni wawili, akiwemo mbunge, katika hafla ya kidini.

Madaktari kupandikiza uume Marekani

Mpiganaji wa zamaniImage copyrightKatarzynaBialasiewicz
Image captionUpasuaji utawezesha mgonjwa kufanya tendo la ngono na kuhifadhi mkojo
Upasuaji umepangwa kufanyika kwa mara ya kwanza kupandikiza uume nchini Marekani, kwa lengo la kuwasaidia mpiganaji wa zamani

Mshindi wa tuzo ya soka ya BBC Afrika kutangazwa

Image captionPeter Okwoche
Tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka inayoandaliwa na BBC, itawekwa hadharani hii leo. Mwandishi wa BBC Peter Okwoche ndiye aliyeteuliwa kukabidhi tuzo hiyo na ndiye mwenye bahasha yenye maelezo ya mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka huu.

Marekani yazidi kuisambaratisha IS

Image copyrightAP
Maofisa wa polisi nchini Marekani wanaoshughulika na mapambano ya kuutokomeza ugaidi, wamesema mkuu wa masuala ya fedha wa kundi la kigaidi la Islamic State ameuawa kutokana na shambulio la anga karibu na mji wa Tal Afar nchini Iraq, katika wiki za hivi karibuni.

Magufuli atangaza baraza la mawaziri

MagufuliImage copyrightStatehouse Tanzania
Image captionDkt Magufuli amesema bado anatafuta watu wa kujaza nafasi nne
Rais wa Tanzania John Magufuli ametangaza baraza lake la mawaziri ambalo kwa sasa lina mawaziri 19, ingawa wizara ni 18. Mawaziri sita kati ya hao ni wanawake.

Mchezaji wa timu ya taifa Honduras auawa kwa risasi


PeraltaImage copyrightAP
Image captionPeralta amewahi kuchezea klabu ya Rangers ya Scotland

Mchezaji wa timu ya taifa Honduras Arnold Peralta amepigwa risasi akiwa likizoni mji wake wa kuzaliwa wa La Ceiba.

01 Desemba 2015

Xi Jinping ziarani Zimbabwe

Image copyrightAP
Image captionXi Jinping akitumbuizwa nchini Zimbabwe
Rais wa China Xi Jinping yuko nchini Zimbabwe katika ziara ya siku mbili inayolenga kujenga mahusiano na Zimbabwe.

Image copyrightReuters
Image captionAsh Carter

Waziri wa ulinzi nchini marekani Ash Carter anasema kuwa kikosi maalum cha jeshi la marekani nchini Iraq kitatumwa kuendesha oparesheni kadha dhidi ya Islamic State nchini Syria.
Bwana Carter aliiambia kamati ya bunge la Congress mjini Washington kuwa kikosi hicho kitafanya mashambulazi, kitawakomboa mateka na kuwakamata viongozi wa Islamic State.

Image copyrightReuters
Image captionMarekani kutuma vikosi maalum Syria

Amesema kwa kwa sasa kuna fursa kubwa ya kuwatenganisha wanamgambo wa Islamic State walioko nchini Iraq kutoka wale walio nchini Syria.
Mwezi Oktoba marekani ilitangaza kuwa itatuma hadi wanajeshi 50 maaalum kwenda kaskazini mwa Syria kama washauri kwa vikosi vya waasi wa Kurdi.

Je umetuma picha za utupu kwa simu? Tahadhari

Image copyrightAP
Image captionJe umetuma picha za utupu kwa simu? Tahadhari
Je umewahi kutuma picha za utupu kwa mpenzi wako ?
Je ulimshawishi akutumie ?

30 wauawa maafisa wa usalama wakipigana Somalia

Shirika la Umoja wa Mataifa linasema watu 40,000 wamekimbia makaazi yao kutokana na mapigano kati ya maafisa wa usalama kutoka maeneo mawili.
Msemaji wa umoja wa mataifa amesema watu 30 wameuawa katika makabiliano hayo yanayoendelea katika maeneo ya Galkayo, eneo lililoko katikati ya Somalia na Puntland Kaskazini .
Kumekuwepo mapigano ya muda mrefu ya kiukoo katika maeneo hayo mawili.
Umoja wa mataifa unasema wakimbizi hao wanahitaji vyakula misaada ya matibabu, maji na huduma za usafi.


KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728