15 Desemba 2015

Utafiti: Uongozi ni ‘hatari kwa maisha

ShinikizoImage copyrightAFP
Image captionShinikizo kutokana na majukumu ya uongozi huenda vinaathiri afya ya viongozi
Utafiti uliofanyiwa afya ya viongozi wa mataifa mbalimbali umebaini huwa wanazeeka haraka na kupoteza miaka mitatu katika muda wao wa kuishi kwa sababu ya uongozi.

Watafiti walichunguza viongozi 279 kutoka mataifa 17, wakichunguza marais na mawaziri wakuu. Miongoni mwa viongozi waliochunguzwa ni kutoka Uingereza, Canada, Ufaransa, Ujerumani na Marekani.
Waliangalia umri wa kufariki kwa viongozi hao wakilinganisha na umri ambao wapinzani wao ambao waliwashinda uchaguzini walifariki wakiwa nao. Muda wao wa kuishi ulishuka kwa miaka mitatu ukilinganisha na wenzao wa umri na jinsia sawa, ambao hawakuwa uongozini.
Madaktari hao walisema mfadhaiko na shinikizo kutokana na uongozi viliathiri sana afya ya viongozi hao.
“Kupoteza miaka kadha ni jambo kubwa sana,” alisema Dkt Anupam Jena kutoka chuo cha matibabu cha Harvard Medical School, ambaye alikuwa mtafiti mkuu katika utafiti huo.
“Labda viongozi walihisi majukumu ya kitaifa yalikuwa na haja zaidi kuliko kula vyema na kufanya mazoezi,” alisema, akiongeza kuwa Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton alikiri kwamba huenda aliishia kula vyakula visivyofaa kutokana na mfadhaiko.
“Labda, kama ulimwengu ungelikuwa na amali, mtindo wake wa maisha ungelikuwa tofauti,” alisema Dkt Jena.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728