15 Desemba 2015

Shule zote Los Angeles zafungwa ghafla

Image copyrightCBS
Image captionShule zote Los Angels zafungwa ghafla
Shule zote za uma katika jimbo Los Angeles Marekani zimefungwa mara moja kufuatia tishio la usalama.

Tangazo hilo lilitolewa na muungano wa wakuu wa shule zote za umma unaathiri takriban shule 1,000.
Takriban wanafunzi laki 700,000 walilazimika kurejea makwao baada ya tishio ambalo kufikia sasa halijatangazwa wazi kupokewa na maafisa wa Polisi.
Yamkini ujumbe wa kuwatahadharisha umma ulipatikana kwa njia ya kielektroniki na hivyo ikawalazimu kuamuru wanafunzi wote waondoke ilikufanikisha shughuli ya kutafuta na kusaka tishio lililoko.
Tahadhari hiyo ya umma imetokea wiki mbili tu baada ya mauaji ya watu 14 katika kituo cha San Bernardino.
Watu hao walipigwa risasi na mume na mkewe ambao wanashukiwa kuwa walishawishiwa na waislamu wenye itikadi kali ughaibuni.
Image captionTakriban wanafunzi laki 700,000 walilazimika kurejea makwao
Polisi tayari wameanza kupekua maeneo yanayoshukiwa kuwa na hatari na wanasema kuwa shule zote zitasalia zimefungwa hadi tishio hilo litakalo ondolewa.
Afisa anayesimamia usalama wa shule za umma Steven Zipperman, amesema kuwa idara hiyo ilipokea tishio kwa njia ya kielektroniki mapema hii leo ndio sababu wakaamuru shule zikafungwa.
''tumeamua kufunga shule hadi pale tutakapobaini kuwa ni salama''
Mmoja wa maafisa wakuu usalama ambaye hakutaka jina lake litajwe anasema kuwa tishio hilo lilipokewa kupitia barua meme iliyotumwa kwa mmoja wa maafisa wanaosimamia shule Los Angeles kutoka ughaibuni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728