16 Desemba 2015

Marekani yapandisha riba baada ya miaka 7

Image copyright
Image captionJanet Yellen Gavana wa Benki Kuu ya Marekani
Benki Kuu ya Marekani imepandisha kiwango kikuu cha riba kwa alama ya robo ya asilimia.

Kwa muda wote tangu mtikisiko wa uchumi nchini humo mwaka 2008 riba ilibaki kuwa asilimia sifuri.
Imekuwa ni kipindi kisicho cha kawaida katika sera za uchumi nchini Marekani na sasa hatua ya benki kuu imeweka alama ya kuanza kurejea kwa kiwango cha riba cha kawaida.
Imechukua takriban miaka saba kwa Benki hiyo kuchukua uamuzi huo wa kuongeza kiwango hicho kidogo cha riba. Hii ni sehemu ya kujikinga na hatari ya mfumuko wa bei kwa siku zinazokuja.
Hata hivyo hatua hiyo sasa inatia mashaka kwa uchumi wa nchi zinakuwa kwa haraka kama Uturuki, Brazili na Afrika Kusini.
Kuna uwezekano kuwa uamuzi huo sasa utawafanya baadhi ya wawekezaji kuondoa fedha zao ili kufaidika na riba hiyo kubwa nchini Marekani.
Pia hatua hiyo itadhoofisha sarafu ya nchi hizo na kuongeza gharama za mikopo.
Aidha pia hatua inatarajiwa kuyumbisha mfumo wa fedha japo nchi tajiri zinaweza kuimarika zaidi kama zitahimilli msukuko huo tafauti na hapo awali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728