03 Aprili 2016

Wenger: Matamshi ya Ozil hayakubaliki

Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa matamshi ya Mesut Ozil kuhusu msimu mbaya wa Arsenal hayakubaliki.

Wenger atazungumza na mchezaji huyo wa Ujerumani anayesema kuwa Arsenal imepoteza fursa ya kushinda taji la Uingereza.
''Nakubaliana kwamba matamshi hayo hayaungwi mkono'' ,alisema Wenger.
''Hata iwapo tuna fursa moja pekee dhidi ya 100 lazima tuamini''.
Ushindi wa mechi tatu kati ya 10 katika ligi ya Uingereza umeiwacha Arsenal ikiwa pointi 11 nyuma ya viongozi Leicester wakiwa na mechi moja ambayo hawajacheza.

Arsenal inakabiliana na Watford siku ya Jumamosi ikiwa ni marudio ya mechi ya kombe la FA ambapo Watford ilishinda na kuibandua Arsenal.
''Kitu kibaya katika maisha ni kutojiamini.Lazima uhakikishe kuwa unajitolea vilivyo na mwishowe ukubali iwapo mpinzani wako ni mzuri kukuliko''.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728