08 Aprili 2016

Liverpool yatoka sare na Dortmund

 
Divock Origi aliifungia Liverpool bao muhimu la ugenini katika mechi yao ya raundi ya kwanza ya nusu fainali dhidi ya Borussia Dortmund ya Ujerumani.

Bao hilo la mshambulizi huyo wa Ubelgiji, lilikuwa pigo kubwa kwa kocha Jurgen Klopp, hasa kwa kuwa Origi alikuwa mchezaji wa zamani wa klabu hiyo.
Hata hivyo kipa wa Dortmund Roman Weifenfeller, aliokoa mkwaju mwingine wa Origi kabla ya Mats Hummels kusawazishia wenyeji.
Juhudi za Dortmund za kufanya mashambulio zaidi katika lango la Liverpool hazikufua dafu pale vijana hao wa Uingereza walipojizatiti na kuzima mashambulio hayo.
Hata hivyo matokeo hayo yalikuwa mema kwa Dortmund, ambayo inapigiwa upato kutwaa kombe hilo la Europa.
Katika mechi zingine Athletico Bilbao walinyukwa mabao mawili kwa moja mbele ya mashabiki wao na klabu ya Sevilla.
Sporting Braga nao walivishwa mabao mawili kwa moja na wageni wao Shaktar Donetsk huku Villarreal ikiwika nyumbani dhidi ya Sparta Prague. Villarreal iliibuka na ushindi wa magoli mawili kwa moja.
Mechi za awamu ya pili ya kombe hilo zinatarajiwa kuchezwa baada ya majuma mawili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728