22 Agosti 2015

Chad:Boko Haram lina kiongozi mpya

 
Rais wa Chad Idriss Deby 
 
Kundi la wapiganaji wa Boko haram kutoka Nigeria huenda limepunguzwa makali kulingana na rais wa Chad Idriss Deby.

Abubakar Shekau siye kiongozi wake tena baada ya mahala pake kuchukuliwa na Mahamat Daoud ambaye yuko tayari kuanzisha mazungumzo na serikali ya Nigeria, alisema rais Deby.
Katika miezi ya hivi karibuni bwana Shekau hajaonekana katika kanda za video za propaganda zinazotolewa na kundi hilo na hivyobasi kuongeza uvumi kwamba huenda ameuawa.
Abubakr Shekau
Mapema mwaka huu vikosi vya Chad vilichukua jukumu kubwa la kuichukua miji na vijiji vilivyotekwa na kundi hilo kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Mwaka uliopita ,kiongozi huyo wa Chad alisemekana kutaka kuanzisha mazungumzo na kundi la Boko Haram ambayo hatahivyo hayakufanyika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728