05 Agosti 2015

China ni haramu kuhifadhi mayai ukiwa hujaolewa

Serikali ya China imepiga marufuku uhifadhi wa mayai kwa wanawake ambao hawajaolewa.
Mjadala mkali umeibuka nchini China baada ya serikali kupiga marufuku kwa uhifadhi wa mayai kwa wanawake ambao hawajaolewa.

Aidha mayai ya wanawake walioolewa wanaweza kuhifadhi mayai iwapo tu wanapata matibabu ya saratani ama matibabu ambayo yatadhuru kizazi chao.
Marufuku ya aina hii si jambo geni kwa raia wa China ambao tayari wanastahimili sheria kali ya kupanga uzazi.
Hata hivyo,ripoti zilipoibuka kuwa muigizaji Xu Jinglei alikwenda Marekani kuhifadhi mayai yake ya uzazi ndipo wachina wakang'amua kuwa huenda sheria hiyo inawalemga maskini.
Maelfu ya wachina wameikashifu sheria hiyo
Maelfu ya wachina wameikashifu sheria hiyo wakisema kuwa ni ya kibaguzi kwa misingi ya jinsia.
Aidha wengine wanahoji kwanini serikali inaingilia kati maswala ya kibinafsi na mambo ya kijamii.
Mjadala huu ulitibuka mwezi Julai baada ya Xu Jinglei alipokiri kuwa ni kweli amehifadhi mayai yake huko Marekani tangu mwaka wa 2013.
Wachina wengi huvuna mayai na kuhifadhi kwa ajili ya kizazi siku za usoni
Muigizaji huyo mwenye umri wa miaka 41 alisema alichukua uamuzi huo kwani hajui ni lini hamu ya kupata mtoto itamwandama.
Siku ya jumapili televisheni ya kitaifa ya CCTV ilitoa ripoti kuhusiana na swala hilo na kuonyesha athari zake na kusema marufuku hiyo haina uhusiano na upangaji uzazi.
Ripoti hii ilisisimua watu katika mitandao ya kijamii ambao wengi wamekuwa wakiitupia dongo serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728