15 Agosti 2015

Al Qaeda:Mwana wa Bin Laden atoa ujumbe

Osama Bin Laden 
 
Kundi la kigaidi la A Qaeda limetoa ujumbe wa sauti ambao unadai kwamba umetoka kwa Hamza Bin Laden ,mwana wa Osama Bin Laden.

Ujumbe huo unaaminika kuwa wa kwanza wa propaganda za Al Qaeda kumshirikisha Hamza Bin Laden kama mwanachama wa kundi hilo.
Katika ujumbe huo uliosambazwa na Al Qaeda katika mtandao wa twitter,Hamza Bin Laden anaagiza mashambulizi dhidi ya Marekani na washirika wake.
Osama bin Laden aliuawa na vikosi maalum vya Marekani mnamo mwaka 2011 katika uvamizi nyumbani kwake huko Abbotabad,Pakistan.
Wanajeshi maalum wa Marekani wakati walipovamia makaazi ya Osama Bin Laden huko Pakistan
Kundi hilo limekuwa likiongozwa na naibu wake Ayman al-Zawahiri.Uwepo wa Hamza Bin Laden haujulikani,anadaiwa kuwa mwenye umri wa miaka ya 20.
Wakati wa uvamizi wa Marekani nchini Afghanistan mwaka 2001,shirika la habari la Al-Jazeera lilionyesha picha yake miongoni mwa wapiganaji wa Taliban nchini Afghanistan.
Ujumbe wake wa sauti uliotolewa na Al Qaeda unawataka wafuasi wake mjini Kabul,Baghdad na Gaza kuanzisha jihad ama vita vitakatifu mjini Washington,London,Paris na Tel Aviv.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728