27 Agosti 2015

Polisi wanasa sehena ya Silaha Kenya

 
Silaha zilizonaswa Garisa
Maafisa wa Ulinzi wa Kenya wamenasa shehena kubwa ya silaha, kufuatia operesheni ya kuwasaka wapiganaji wa Al Shabaab Kaskazini mwa Kenya.

Idara ya polisi imesema kuwa maafisa wake walinasa risasi, vilipuzi, bunduki na vifaa vinavyotumika kutengeneza mabomu ambazo zinaaminika kuwa ya wapiganaji wa Harakat walio na uhusiano na kundi la Al Shabaab nchini Somalia.
Wapiganaji kadhaa wa kundi hilo ambao walikuwa wakisafirisha silaha hizo, walikamatwa na wanazuiliwa na maafisa wa polisi.
Kundi hilo linasemekana kuwa na majukumu ya kuwasilisha na kutoa mafunzo kwa wapiganaji wapya na hatya kujiunga na mapigano na mashambulio dhidi ya vituo vya umma.
Kukamatwa kwa shehena hiyo ya silaha ni pigo kubwa kwa kundi hilo la al-Shabaab. Katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita wapiganaji wa al shabaab wamejaribu kuingiza silaha na kufanya mashambulio nchini Kenya.
Maafisa wa ulinzi na upelelezi nchini Kenya wameimarisha juhudi zao ya kupambana na kundi hilo kwa kuwakamata washukiwa wa kundi hilo na hata kushambulia kambi zao.
Wapiganaji kadhaa wa kundi hilo kwa sasa wanazuiliwa na polisi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728