31 Desemba 2014

Kwa heri mwaka 2014 ulionogeshwa na filamu ya Katiba na Escrow

Hatmaye miezi 12 imekamilika leo ikiashiria kumalizika kwa mwaka 2014 utakaokumbukwa na wengi kwa kuwa na matukio motomoto.

TMA yatahadharisha wananchi kuhusu ongezeko la joto

Dar es Salaam. Mvua kubwa isiyotabirika inatarajiwa kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini hasa katika ukanda wa Pwani ya Kaskazini, maeneo ya Dar es Salaam, Tanga, Unguja na Pemba; pia katika ukanda wa Kaskazini Mashariki kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

Dereva wa bodaboda auwawa kinyama

Tanga. Watu wasiojulikana wamevamia nyumba ya dereva wa bodaboda, Omari Shaaban (32) na kumuua kisha kuichoma moto, katika tukio linalohusishwa na visa na wivu wa mapenzi.

Siku za wauza unga zahesabika china

Dar es Salaam. Siku za wasafirishaji na wauzaji wa dawa za kulevya kwenda China sasa zinahesabika baada ya Jeshi la Polisi na kitengo chake cha Dawa za Kulevya kubaini majina ya vigogo wanaofanya shughuli hiyo na kusema imeanza kuwashughulikia kimyakimya.

30 Desemba 2014

Dk. Slaa, polisi wapambana Dar

slaaHALI ya tafrani ilizuka jijini Dar es Salaam jana, baina ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa na askari wa Jeshi la Polisi.

Pengo aonya ufujaji wa Escrow

pgIKIWA imebaki miezi 10 kufikia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amewataka Watanzania walio masikini kuungana ili kuwang’oa madarakani viongozi matajiri wasiojali maslahi ya taifa.

Nyalandu atangaza kugombea urais

Pg 3.MBIO za urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimechukua sura mpya baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, kutangaza rasmi nia ya kugombea urais mwaka 2015.

25 Desemba 2014

Kambi ya jeshi la AU yavamiwa Somalia

Wapiganaji wa Al shabaab wamefanya shambulizi katika kambi kuu ya jeshi la Umoija wa Afrika karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu Somali.

Indonesia wakumbuka Tsunami

Wananchi wa Indonesia wameanza kuadhimisha mwaka wa kumi tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi lililosababisha mawimbi makubwa katika bahari ya Hindi, tsunami na kusababisha vifo vya watu zaidi ya watu laki mbili na elfu ishirini katika eneo kubwa.

Mtu aliyetabiri mwisho wa dunia afariki

Kiongozi mmoja wa dini ambaye alipata umaarufu nchini Kenya kwa kutabiri mwisho wa dunia mwaka 2006 amezikwa katika kijiji cha Bomet.

Filamu yenye utata yawekwa mitandaoni

Kampuni ya Sony Pictures imesema kuwa sinema yenye utata ya ucheshi kuhusu namna ya kumuuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, imewekwa katika mitandao Nchini Marekani.

24 Desemba 2014

Ajali

Ajali ya gari yachukua maisha ya wawili papo hapo muda mfupi uliopita huko Nzega. Chanzo chadaiwa ni mwendo kasi na mvua.

usajili wa Messi mtihani kwa Chelsea

Kocha wa Timu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kwa sasa hawana nafasi ya kumsaini mchezaji Lionel Messi kwa kuwa hakuna Fedha ya kutosha kumsajili mchezaji huyo .

Matic asema Chelsea itashinda mataji 4

Mchezaji wa kilabu ya Chelsea Nemanja Matic amesema kuwa anaamini kuwa kilabu hiyo itashinda mataji manne msimu huu.

Waziri mkuu mpya aidhinishwa Somali

Bunge la Somalia limeidhinisha uteuzi wa waziri mkuu mpya akiwa ni afisa wa tatu kuhudumu katika wadhfa huo katika kipindi cha miaka miwili.

Frank Lampard kusalia Manchester City

Bosi wa Manchester City Manuel Pellegrini anaamini watambakisha kiungo Frank Lampard.

IS:Yadungua ndege ya jeshi la muungano

Wapiganaji wa Islamic State nchini Syria wamedai kuidungua ndege ya kivita ya muungano wa jeshi unaoongozwa na Marekani.

Sakata la Escrow bado

Nchini Tanzania mtikisiko wa matokeo ya kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow umeendelea baada ya Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi kusimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake. Maswi anakuwa kiongozi wa tatu wa ngazi ya juu kukumbwa na upepo huo akitanguliwa na Mwanasheria mkuu wa serikali ambaye alijiuzulu mwenyewe na Waziri wa Ardhi aliyetimuliwa kazi hadharani na Rais Jakaya Kikwete. Licha ya kuondoka kwa viongozi hao bado baadhi ya wananchi na vyama vya upinzani wameendelea kulalamika kuwa juhudi za kutekeleza maazimio ya Bunge ni ndogo. Kuhusiana na hilo Baruan Muhuza wa BBC alizungumza na Neville Meena, katibu wa Jukwaa la wahariri Tanzania.

Suarez atoa zawadi ya krismasi

mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez ametoa zawadi kwa watoto 500 na familia zao.

Vilabu vya Ulaya na Tetesi za usajili .

Uongozi wa Timu ya Manchester United umesema upo tayari kutoa paundi milioni 120 kwaajili ya kumsajili winga Gareth Balle mwenye umri wa miaka 25 kwa mwezi januari kutoka klabu ya Real Madrid , winga ambaye ni miongoni mwa wachezaji ghali zaidi ulimwenguni.

23 Desemba 2014

Ufisadi: mwingine asimamishwa Tanzania

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, amemsimamisha kazi kwa muda , Eliakim Maswi, Katibu Mkuu ya Wizara ya Nishati na Madini, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake, kama ilivyoelekezwa na Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.

Mpia njia aeruhiwa kwa risasi

Mpita njia ajeruhiwa kwa Risasi na Majambazi waliovamia na kupora ktk duka la Pesa Morocco, Kinondoni - Dar
- Majambazi walivamia kiduka cha M-PESA, tiGO PESA na Airtel Money; wakati wanaondoka wakawa wanapiga risasi ikampata huyu dada aliyekuwa anapita barabarani hajui hili wala lile

22 Desemba 2014

Michael Carrick ni mchezaji bora

Kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema Michael Carrick ndie mchezaji bora wa kingereza kwa sasa.

Korea kazkazini sasa yaionya Marekani

Korea Kazkazini sasa inataka uchunguzi wa pamoja na Marekani kufanywa kuhusu wizi wa mtandaoni uliosababisha kampuni ya Sony Pictures kuahirisha maonyesho ya filamu ya ucheshi inayomdhihaki raia wa Korea kazkazini Kim Jong-un.

Rais Kikwete amfukuza kazi Profesa Tibaijua, Muhongo awekwa kiporo

Rais wa Jamhuri wa Tanzania Jakaya Kikwete ametangaza kutengua uteuzi wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka baada ya vyombo vya Serikali kubaini na kijiridhisha kuwa amekiuka maadili ya utumishi wa Umma kwa kuingiziwa fedha kiasi cha Sh1.65bilioni kwenye akaunti yake binafsi.

Matokeo darasa la saba sasa hadharani

Beatrice Moses na Ibrahim Yamola
SERIKALI imetangaza matokeo ya darasa la saba mwaka huu, huku takwimu za matokeo hayo zikionyesha kuwa zaidi ya nusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2013 ni wale waliopata asilimia 40 ya alama kwenda chini katika matokeo hayo.

Jaji Warioba apigwa vita

Mwanza. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba amesema licha ya kushambuliwa kwa mambo ya msingi anayozungumza kuhusu Katiba Mpya hakuna mtu aliyejitokeza kumjibu hoja zake, zaidi kumpiga vita kwa kutumia njia wanazo jua.

Mshtakiwa wa EPA, aachiwa huru na Mahakama

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru Johnson Lukaza na mdogo wake Mwesigwa Lukaza baada ya kuwaona hawana hatia katika kesi ya wizi wa  wa Sh 6.3 bilioni za akaunti ya madeni ya Nje (EPA) iliyopo Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kitendawili cha Escrow: Chadema yaongeza orodha

Dar es Salaam. Masikio ya Watanzania leo yameelekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete watakapokuwa wakisikiliza hotuba yake kwa Taifa inayotarajiwa kujibu maswali yapatayo 10 ambayo yanatarajiwa kutegua kitendawili cha kashfa ya uchotaji wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow.

Bibi amuua mjukuu wake kwa kumtupa nje ya basi kupitia dirishani

Dar/ Singida. Jeshi la Polisi mkoani Singida, linamshikilia Nawaridi Saidi (45), mkazi wa Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtupa mjukuu wake Mayasa Meshack (6) kutoka ndani ya gari wakati akisafiri kwenda Kigoma akitokea Dar es Salaam.

21 Desemba 2014

Jaji Warioba aunguruma Mwanza, ataka majibu ya hoja zake

Mwanza. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba amesema licha ya kushambuliwa kwa mambo ya msingi anayozungumza kuhusu Katiba Mpya hakuna mtu aliyejitokeza kumjibu hoja zake, zaidi kumpiga vita.

Mgombea CCM atangazwa mshindi kabla ya kura, Chadema wagoma, vurugu zazuka

Mwanza. Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakazi wa Mtaa wa Ibungilo B, Kata ya Ibungilo, Wilaya ya Ilemela mkoani hapa, wamekumbwa na hali ya sintofahamu wakati wakijianda kupiga kura ya kumchagua Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo, baada mgombea wa nafasi hiyo kupitia CCM kutangazwa mshindi kabla ya wao kupiga kura.

18 Desemba 2014

Wanajeshi wa Nigeria wahukumiwa kifo

Mhakama moja ya kijeshi nchini Nigeria imewahukumu kifo askari 54 kwa kukataa kupigana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Boko Haram.
Chelsea are set to spend £40 million to bring this Real Madrid star to the club in January!! This will be AMAZING!! 

Chelsea Transfer Gossip

   Eden Hazard - N/A

  Eden Hazard is set to sign a new five-year contract with Premier League leaders Chelsea that would make the Belgium international the club’s highest-paid player.

Kikwete kutegua kitendawili Escrow?

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete leo atalihutubia taifa la nchi hiyo ambapo anatarajiwa kuyatolea ufafanuzi masuala nyeti yanayoligusa taifa hilo.

14 Desemba 2014

NANI MTANI JEMBE NDO HABARI YA MJINI



Aguero nje kwa mwezi mmoja

NI sawasawa na Barcelona kucheza bila ya Lionel Messi au Real Madrid kucheza bila ya Ronaldo. Manchester City wanatazamiwa kuwa na kibarua kigumu baada ya habari kuwa staa wao, Sergio Aguero atakuwa nje kwa mwezi mzima.

Ronaldo na Messi

SUPASTAA, Cristiano Ronaldo Jumamosi iliyopita alipiga ‘hat-trick’ yake ya 23 kwenye La Liga na kuweka rekodi wakati alipoiongoza Real Madrid kuichapa Celta Vigo mabao 3-0.

Wanafunzi 826 na walimu wao wakimbia vita Kiteto

Siku kadhaa zimepita tangu kutokea kwa mapigano mapya kati ya wakulima na wafugaji katika Wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara.

Kivumbi Uchaguzi Serikali za Mitaa

Dar es Salaam. Watanzania leo wanaingia kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliofunikwa na malalamiko kadhaa ya ukiukwaji wa kanuni, huku chama tawala CCM na wapinzani wakitambiana kushinda.

Serikali ya awamu ya nne kumaliza vibaya’

Dar es Salaam. Wakati Serikali ya Awamu ya Nne imebakiza takriban mwaka mmoja kuondoka madarakani, sifa ya Tanzania kwenye jumuiya ya kimataifa imeendelea kutiwa doa kutokana na kuhusishwa na ongezeko la ufisadi wa mabilioni ya fedha za umma na ujangili.

Wapinzani walia CCM kuwachezea rafu

Dar es Salaam. Vyama vya CUF na Chadema vimekitupia lawama Chama cha Mapinduzi (CCM) vikidai kimecheza rafu katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaofanyika leo.

Necta yatangaza mfumo mpya

Dodoma. Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limeanza mfumo mpya wa kupanga matokeo ya kidato cha nne mwaka huu na ya kidato cha sita mwakani, ambapo sasa madaraja yatapangwa kwa wastani wa pointi (GPA) badala ya jumla ya pointi.

13 Desemba 2014

JINSI YA KUPATA ARDHI KIAHERIA SEHEMU YA KWANZA

Ardhi ni mali na watu wanajipatia ardhi kwa njia mbalimbali. Leo tutaangalia njia mbadala ambazo watu hujipatia ardhi hapa nchini.

Karatasi za kupigia kura zanaswa D’Salaam

Dar es Salaam. Wakati Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ukitarajiwa kufanyika kesho nchi nzima, wafuasi wa (Chadema) na Jeshi la Polisi, wamekamata karatasi zinazodaiwa za kupigia kura kwenye uchaguzi huo za Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, zikirudufiwa jijini Dar es Salaam.

Zitto apeleka moto wa kufichua ufisadi kwa wawakilishi Z’bar

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe amewataka wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanaounda kamati hiyo, kufanya kazi kama ilivyo kamati yake kwa Tanzania Bara.

Marekani yacharuka escrow;Tanzania yakosa mabilioni ya MCC, ni Dola 450 milioni

Dar es Salaam. Wakati Serikali ya Marekani ikisema haitatoa fedha za Changamoto za Milenia (MCC) hadi utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu ufisadi katika akaunti ya Tegeta Escrow wa Sh306 bilioni utakapofanyiwa kazi, Ikulu imesema, Rais Jakaya Kikwete hatatekeleza agizo hilo kwa shinikizo la msaada huo.

NEC wataka JWTZ, Ukawa wapinga

Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imetaka uboreshwaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura usimamiwe na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

TRA: Watumishi waliotajwa kashfa ya escrow wako kazini

Dar es Salaam. Watumishi wawili wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), waliotajwa katika kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow wanaendelea na kazi wakisubiri taratibu za utumishi wa umma kabla ya kuchukuliwa hatua.

MAMBO YA MTANI JEMBE HAYO


11 Desemba 2014

Kikwete kuamua IPTL ndani ya wiki

Dar es Salaam. Siku moja baada ya Ikulu kueleza kuwa Rais Jakaya Kikwete pamoja na kupokea ripoti kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow hawezi kuwachukulia hatua wahusika mpaka uchunguzi kuhusu suala hilo utakapokamilika, ofisi hiyo ya Rais sasa imesema atafanyia kazi uamuzi wa ripoti hiyo katika wiki moja ijayo.

10 Desemba 2014

JK akagua gwaride la mwisho la Uhuru

Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete jana alikagua gwaride la Uhuru la vikosi vya ulinzi na usalama ambavyo baadaye vilipita mbele yake kutoa heshima ikiwa ni maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanganyika.

08 Desemba 2014

Diamond kuwa mgeni rasmi ‘Zari All White Ciroc’

Licha ya kumzidi miaka 10, Zari atangaza rasmi kuwa ni mtu wake wa karibu kwa sasa.
Johannesburg/Dar. Baada ya kuukimbia ukweli kwa kipindi cha mwezi mmoja, mwanamuziki Diamond Platnumz amethibitisha kuwa na uhusiano baina yake na staa maarufu kutoka Uganda, Zari ‘The Boss Lady’ na kwamba atakuwa mgeni rasmi katika hafla yake ijulikanayo ‘Zari All White Ciroc’ itakayofanyika mwezi huu.
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728